Dereva wa jaji EACJ auawa
Dereva wa mmoja wa majaji wa Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACJ), Ibrahim Msagati amefariki dunia kwa kupigwa risasi iliyofyatuka kutoka kwenye bastola ya mlinzi wa jumuiya hiyo.
Tukio hilo lililoibua majonzi na simanzi miongoni mwa wafanyakazi wa EAC lilitokea jana saa saba mchana muda mfupi baada ya kikosi cha ulinzi cha Jumuiya kumtia mbaroni mtu mmoja aliyefika Makao Makuu ya EAC kwa tuhuma ambazo hazikujulikana mara moja.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Lebaratus Sabas alisema tukio hilo ni la bahati mbaya kwani risasi ilifyatuka kutoka kwenye silaha ya mmoja wa maofisa usalama wa EAC.
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya Umma wa EAC, Richard Otieno-Owora alimtaja ofisa usalama ambaye risasi ilifyatuka kutoka kwenye bastola yake kuwa ni Jackson Oula.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina gazetini, mmoja wa wafanyakazi wa Sekretarieti ya EAC alisema risasi hiyo ilifyatuka wakati ofisa huyo akijaribu kutoa simu maalumu ya kiusalama waliyotumia kunasa mawasiliano ya mtu waliyemtia mbaroni ili kuwapa ushahidi polisi waliokuwa wakichukua maelezo yao.
"Wakati akitoa simu mfukoni, risasi aliyoiweka chemba wakati wa kumtia mbaroni mtuhumiwa ilifyatuka na kutoboa kiti alichokalia mfanyakazi mwenzetu na kumpiga mgongoni na kusababisha kifo chake," alisema.
Dereva huyo aliajiriwa hivi karibuni na alikuwa akiendesha gari inayotumiwa na Jaji Mfawidhi wa EACJ, Jean-Bosco Butasi.
Chanzo: Mwananchi
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments