[wanabidii] TAARIFA YA POLISI KUHUSU VIKUNDI VYA MBWA MWITU

Saturday, May 24, 2014
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI 
Kufutia kuibuka kwa vikundi vya vijana vinavyojulikana kwa majina ya mbwa mwitu, watoto wa mbwa au Panya road na kujihusisha na vitendo vya kihalifu ikiwemo uporaji, unyang'anyi wa kutumia nguvu na kujeruhi watu katika maeneo mbalimbali jijini Dar es salaam,
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi (DIGP) Abdulrahaman Kaniki amewaagiza makamanda hususani wa Kanda Maalumu ya Dar es salaam kuhakikisha wanavitafuta vikundi hivyo popote vilipo, kuwakamata na kuwafisha katika vyombo vya sheria.
Naibu IGP amekemea vikali vikundi hivyo na kuvitaka kuacha tabia hiyo mara moja, kwani vitendo hivyo ni vya kihalifu na vinatakiwa kukemewa na kila mtu katika jamii.
Aidha, amewataka wananchi kuondoa hofu na badala yake watoe ushirikiano kwa kutoa taarifa za vikundi hivyo katika vituo vya Polisi ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa.
Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments