Ndugu zangu,
Kwenye jamii yeyote ile, pasipo na uhuru wa kujieleza na pasipo na utii wa sheria, basi, hakuna demokrasia.
Kila mtu aweze kusema kwa uhuru kabisa. Na si kusema tu, asikilizwe anachosema. Hata kama mawazo yake hayapendwi kiasi gani.
Wenye fikra tofauti, hata wakiwa wachache ni vema wakasikilizwa. Ni haki yao. Fikra zao ziruhusiwe na zishindwe tu kwenye majadiliano ya hoja. Na hata wakishindwa kwa hoja, uhuru wao wa kuendelea kujadili jambo waliloshindwa lazima uheshimiwe na ulindwe. Maana, wachache hao wanaweza kuyapanga upya mawazo yao na hata kufanikiwa kuwashawishi walio wengi kukubaliana nao.
Na walio wengi nao wana haki ya msingi ya kuyasimamia mawazo yao hata pengine kuwaridhisha wachache kuwa kilichoamuliwa kwa mawazo ya wengi ni sahihi. Maana, siasa ni majadiliano endelevu ya hoja na si kugombana kwa kutiana kabali au kutishana.
Na katika kulumbana huko kwa hoja kuna wakati lazima kulumbana huko kukatishwe na maamuzi yafanyike. Bila hivyo hakutakuwa na kazi yoyote inayofanyika isipokuwa kulumbana tu.
Kama ilivyo, kuwa walio wachache ni vema wakasikilizwa, mawazo ya walio wengi hayana budi pia kuheshimiwa. Maana, uamuzi utakaotolewa utakuwa umetokana na mawazo ya walio wengi. Utakuwa ni uamuzi wa watu na si kikundi kidogo cha watu.
Na kwa vile maamuzi yenye kutokana na matakwa ya wengi ndio yenye kufanya sheria, basi, la pili la muhimu katika demokrasia ni utii wa sheria. Ni lazima kila mmoja atii sheria, ni pamoja na wale walioipinga kabla ya kupitishwa na wengi kwa kufuata misingi ya kidemokrasia.
Ni Neno Fupi La Usiku.
Maggid Mjengwa,
Iringa.
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la ‘Mabadiliko’.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
To view this discussion on the web visit https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/CAMD-ye7uPWYAZV08UYvVSd69DeCSX5-5GDFfo1yMh--m3%3D3u%3DA%40mail.gmail.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments