[wanabidii] SPIKA WA BUNGE LA KATIBA ,CHENGE NI BORA KULIKO SITTA

Monday, February 17, 2014
kwa  maoni yangu mbunge wa bariadi mashariki  Andrew Chenge  ni bora  kulko Samwel Sitta  kuongoza  bunge la katiba.

sababu  ni kwamba Sitta ni waziri kwa hiyo ni mtu w a serikali  wapinzani w atalalamika, pili Sitta  anachembe chembe za kugombea urais hivyo  mawazo yake yatalenga  kusimamia sifa za  mgombea  ambazo  anazoyeye huku  akisimamia vipengele  ambavyo vinawanyima wenzake hak ya kugombea.

hatuhitaji katiba kama hiyo wala spika kama huyo, Chenge  hana nia  ya urais  atasimamia  katiba  ya wote , itapendeza kama chenge atasimamia  katiba inayolinda  dola sio katiba inayoshabikia  mapinduzi  au kuanguka  kwa dola  jambo  analoweza kulifanya Sitta.

kwasababu hadi sasa Sitta hajawa na uhakika wa chama gani  atagombea hivyo ni rais kusimamia katiba inayoegemea  upinzani  dhidi  ya  dola jambo  ambalo litasababisha chama kingine kungia  madarakani  serikali itaingia gharama  za kubadili tenda katiba .

DEMOKRASIA  BILA  NIDHAMU NI UASI.   

Share this :

Related Posts

0 Comments