[wanabidii] Mafunzo ya Kuweka Akiba kwa Wanafunzi Kibasila

Saturday, October 12, 2013
CODE....

TPB Yatoa Mafunzo ya Kuweka Akiba kwa Wanafunzi Kibasila

<a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/Wanafunzi-Kibasila.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-38778" alt="Wanafunzi Kibasila" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/Wanafunzi-Kibasila.jpg" width="640" height="465" /></a>

<a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/Picture-020.jpg"><img class="aligncenter size-large wp-image-38782" alt="Picture 020" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/Picture-020.jpg" width="500" height="320" /></a>
<p style="text-align: center;"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/Picture-052.jpg"><img class="aligncenter size-large wp-image-38783" alt="Picture 052" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/Picture-052.jpg" width="500" height="333" /></a>
Picha mbalimbali juu ni baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kibasila ya jijini Dar es Salaam wakiwa katika banda la Benki ya Posta Tanzania (TPB) wakifungua akaunti maalumu ya mwanafunzi 'Platinum Account' baada ya kupewa elimu shuleni hapo.</p>
<p style="text-align: center;"></p>
<a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/IMG_0012.jpg"><img class="aligncenter size-large wp-image-38781" alt="IMG_0012" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/IMG_0012.jpg" width="500" height="336" /></a>

&nbsp;
<p style="text-align: center;">Baadhi ya maofisa wa TPB (kulia) wakitoa maelezo kwa wanafunzi na kuwafungulia akaunti wanafunzi walipowatembelea shuleni hapo kutoa elimu.</p>
<a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/IMG_0007.jpg"><img class="aligncenter size-large wp-image-38787" alt="IMG_0007" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/10/IMG_0007.jpg" width="471" height="640" /></a>

&nbsp;
<p style="text-align: center;">Meneja Mkuu Ukuzaji Amana wa Benki ya Posta Tanzania, Paradise Nkini (kushoto) akizungumza na vyombo anuai vya habari.</p>
<strong>Na Joachim Mushi, Dar</strong>

<strong>BENKI</strong> ya Posta Tanzania (TPB) leo imepeleka huduma na elimu juu ya akaunti maalumu ya wanafunzi ujulikanayo kama 'Platinum Account' kwa wanafunzi wa kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Kibasila ya jijini Dar es Salaam. Mbali na huduma hiyo wanafunzi hao pia walifundishwa umuhimu wa kujiwekea akiba

Akizungumza kutoa elimu kwa baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo, Meneja Mkuu Ukuzaji Amana wa TPB, Paradise Nkini alisema TPB imeadhimia kutoa elimu kwa wanafunzi hasa kidato cha tano na sita ili kuwajengea mazoea ya kuanza kujiwekea akiba hali ambayo itawasaidia hapo baadaye.

Alisema kwa mipango ya sasa TPB itatoa elimu kama hiyo katika shule za sekondari ya mikoa ya Dar es Salaam na Pwani na baada ya hapo elimu kama hiyo itaendelea kutolewa mikoa yote. Alisema elimu hiyo ya kujiwekea akiba kwa wanafunzi inayotolewa na benki hiyo inatolewa sambamba na huduma ya 'Platinum Account' ambayo ni akaunti maalumu kwa wanafunzi iliyoandaliwa kumudu mazingira ya mwanafunzi.

"Tumekuja pia kutambulisha akaunti yetu maalumu kwa wanafunzi ijulikanayo kama Platinum, hii imeandaliwa kwa ajili ya wanafunzi na imezingatia kipato chao...kwanza inafunguliwa kwa sh. 5,000 tu, haina makato ya kila mwezi na haina gharama za uendeshaji kama ilivyo kwa akaunti nyingine," alisema Nkini.

Aidha alisema sambamba na elimu inayotolewa kwa wanafunzi, TPB inatoa zawadi kwa baadhi ya shule zilizofanya vizuri kitaaluma na kuwazawadia wanafunzi baadhi ya vifaa vinavyowasaidia katika masomo yao.

"...Tunatoa zawadi kwa baadhi ya shule hasa zilizofanya vizuri na zile shule ambazo zinahali ngumu za vijijini, tunatoa zawadi za madaftari, tunatoa kalamu na kuwashirikisha wananfunzi waweze kuelewa benki yao vizuri," alisema Nkini akizungumza na wanahabari kwenye viwanja vya shule ya Kibasila.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
_____________________________________________________________________
Joachim Mushi, Mhariri Mkuu wa gazeti tando la Thehabari.com
Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com
Mobile:- 0717 030066/ 0786 030066/ 0756 469470
Web:- www.thehabari.com  
          http://joemushi.blogspot.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments