[wanabidii] Tamasha waandishi-Taswa Queen kutoka Dar yatwaa ubingwa

Monday, September 09, 2013

Mwandishi Wetu, Mwananchi

Arusha: Timu ya Mpira wa pete (netball) ya wanahabari wa jijini Dar es Salaam,Taswa Queen   juzi ilitwaa ushindi katika bonanza la nane la Waandishi mkoa wa Arusha, baada ya kuichapa timu ya chuo cha uandishi wa habari Arusha Arusha(AJTC) magoli 21-1.

Wakati Taswa Queen wakitwaa ubingwa kaka zao, TASWA SC , walishindwa kunyakuwa kombe, baada ya kutoka suluhu na timu ya AJTC katika mchezo mkali wa fainali, ambao ulisitishwa kutoka na kiza wakati wa mikwaju ya penati timu hizo, zikiwa zimefungana 1-1.

Kutokana na matokeo hayo, Meneja wa kampuni ya Tanzania Breweries Limited(TBL), Endrew Warden alimkabidhi Meneja wa Taswa Majuto Omar fedha taslim 200,000/= na meneja wa AJTC Modaha Lucas alikabidhiwa kiasi cha sh 200,000/=

Taswa dar, walifanikiwa kuingia fainali baada ya kuichapa timu ya Radio 5 magoli 3-1 na baadaye kuifungua timu ya Arusha 1-0 katika mchezo mkali wa nusu fainali.

Kwa Upande wa AJTC, waliingia fainali baada ya kuichapa timu ya  Taswa Arusha, 1-0 na baadaye waliwatoa Sunrise radio kwa penati 11-12 baada ya timu hizo kutoka sale.

Katika mchezo wa fainali ya mpira wa pete   uliochezwa uwanja wa general Tyre jijini Arusha, Taswa Queen waliwadhibiti kila idara, AJTC ambao walikuwa ni mabingwa watetezi.

Kutokana na ushindi huo, Taswa Queen walikabidhiwa kikombe na Meneja mauzo wa kampuni ya Megatrade, Gudluck Kway na fedha taslimu 150,000.

Katika michezo mingine, timu ya ORS kutoka Manyara, ilifungwa  na Sunrise 2-1 na baadaye ORS iliwafungua TBL Arusha goli 1-0 na hivyo kutwaa zawadi ya timu yenye nidhamu.

Katika tamasha hilo, katika mchezo wa kuku, wanahabari kutoka Taswa Dar es Salaam, AJTC na Taswa Arusha walitamba na kushinda.

Tamasha hilo la nane la vyombo vya habari mkoa wa Arusha, liliandaliwa na TASWA Arusha kwa ushirikiano na kampuni ya Ms Unique na kudhaminiwa na TBL,TANAPA, Megatrade,AICC,Cocacola, Pepsi na Wazee Klabu.

MWISHO.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments