Ndugu zangu,
Ni bahati mbaya sana kuwa tumewekeza katika uongo. Tumekuwa waongo mno. Tuna wanasiasa waongo. Tuna viongozi wa dini waongo na tuna hata wanahabari waongo.
Na duniani hapa kuna aina tatu za uongo; Mosi, kuna uongo wa kawaida usio na madhara sana, hata kama ni jambo baya. Kwa mfano, utamkuta mtu mmekaa nae Kijitonyama, basi, ataongea na mke au mumewe kuwa yuko Mbagala Rangi Tatu! Sasa Kijitonyama na Mbagala Rangi Tatu wapi na wapi! Lakini hakuna atakayekufa kwa uongo huo hata kama ni kitu kibaya.
Pili, kuna uongo wa Kitakwimu. Kwamba takwimu zinatumika kuongopa. Kiongozi anasimama na kuwasomea wananchi takwimu bila uthibitisho. Na kwa vile wengi hatujui hesabu, basi, tunaishia kuongopewa.
Tatu, uongo wa kishetani. Huu ni uongo mbaya kuliko wote. Watu wanaongopa kwenye mambo ya msingi yenye kuhusu mustakabali wa taifa, mtu binafsi na hata afya na uhai wa watu.
Kwa mfano, nesi aliyeambiwa na daktari ampe vidonge mgonjwa aliye taabani kitandani. Lakini kwa vile ndugu wa mgonjwa hawakuacha chochote kwa nesi, mgonjwa ataachwa. Na akifa bado akiulizwa nesi atasema kwa macho makavu kuwa amempa mgonjwa dawa lakini hazikufanya kazi! Nesi hapa ameongopa. Na huu ni uongo wa kishetani wenye kupelekea mauti ya mwanadamu mwingine.
Naam, tumewekeza katika uongo. Tumekuwa waongo mno. Tubadilike.
Maggid.
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda; mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com
Utapokea Email ya kudhibitisha kujiondoa kwako.
TEMBELEA Facebook yetu:
http://www.facebook.com/MabadilikoForums?ref=hl
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forums" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 Comments