[wanabidii] Tahadhari kwa taifa

Tuesday, August 20, 2013
Naomba ndungu msichange matokeo na misimamo ya vyama vingi na umoja wa wananchi katika masuali mbali mbali ya kimsingi. Sidhani kama kuna chama chochote kinachokubaliani na aina yoyote ya uhalifu kama kuchoma makanisa, misikiti, nyumba za watu, kupigana mapanga, kuuwana, kumwagiana tindikali nk. Ni sisi wananchi wenyewe ndio tunafanya mambo hayo. Nani tunapaswa kumlaumu? Kisheria na kisiasa tunatakiwa kuilaumu SERIKALI ambayo inaongozwa na chama tawala-CCM kwa mabaya yote yanayotokea. Iwapo upinzani utakuwa mzuri na wenye busara raia wataelewa vyama vyao vina msimamo gani. Umoja nchini Tanzania upo. Kinachokosa ni upungufu wa watu wa kawaida kuelewa malengo halisi ya vyama vyao na ni hapo ndio ccm wanajiona Miungu watu
Historia inatufundisha kuwa kuanzia enzi za ukoloni ( dutch ostafrica) nchi yetu ilikuwa imezunguukwa na maadui. Rwanda na Burundi baadae wakatolewa na tukajiunga na wisiwa ambavyo pia vilikuwa chini ya himaya ya maadui zetu. Leo chokochoko zote hizo tunaziona pande zote magharibi,mashariki, kaskazini na kusini mwetu (Malawi). Enzi za Mwl. Nyerere tulikuwa na chama kimoja tu, leo tuna vyama vingi, hiyo sauti zimekuwa nyingi kiasi kwamba zinaleta chuki kwa baadhi yetu. Wanaotawala hawataki kukoselewa na wapinzani wao, kwa njia hiyo umoja mnaosema ndio unaonekana haupo. Hayo ni baadhi tu ya matokea ya demokrasia.
Tunachotakiwa sisi kufanya ( especially for us intelectuals) sio kuwakosoa viongozi wetu katika masuala ya kimataifa. Hayo ya ndani tunaweza kukosoana sana. Kwa mfano,kusema kuwa hatuwezi kushinda vita hata kanakwamba tuna jeshi kubwa kunamuongezea jeuri Mnyarwanda ambaye atasoma tuuandikavyo. Umoja ni sisi sote tunapaswa kuuimarisha. Tuna methali nyingi zinazo ongelea umoja, kidole kimoja hakivunji chawa.
Mtanganyika

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments