UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
Academic Staff Assembly

24/7/2013
Mwaliko kwenye Kongamano la UDASA Kuhusu Amani na Usalama wa Taifa Letu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 28/7/2013
Kwa niaba ya Uongozi wa Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, napenda kukukaribisha kwenye kongamano la kujadili Amani, Ulinzi na Usalama wa Taifa litakalofanyika tarehe 28/7/2013 ndani ya ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia saa 8 mchana hadi saa 12 jioni. Kongamano hilo litarushwa moja kwa moja na ITV.
Mada kuu ya kongamano hilo ni, "Mustakabali wa Amani na Usalama wa Wananchi na Taifa Letu kwa Miaka 50 ijayo". Katika Mada hii kutakuwa na vipengele vikuu vitatu vitakavyojadiliwa:
a) Mchango wa Vyombo vya Dola katika Amani na Utulivu wa taifa letu;
b) Mchango wa Siasa na Dini katika kuimarisha Amani na Usalama wa Taifa letu;
c) Mchango wa Vyombo vya Habari katika kuimarisha au kubomoa Amani na Usalama wa taifa letu.
Tutanguliza shukrani zetu za dhati kwa ushiriki wako kwenye kongamano hili.
Asante
Faraja Kristomus
(Katibu – UDASA)
Mr. Faraja Kristomus
Department of Foreign Languages and Linguistics
University of Dar es Salaam
P.O.Box 35040, Dar es Salaam
Tanzania
Mobile: +255 787 52 53 96 / +255 717 086 135
"All human beings are equal except our beliefs, tribes and thinking, which are always accidents and never the essences of our humanity. We acquire them after getting out of the wombs of our mothers".
Department of Foreign Languages and Linguistics
University of Dar es Salaam
P.O.Box 35040, Dar es Salaam
Tanzania
Mobile: +255 787 52 53 96 / +255 717 086 135
"All human beings are equal except our beliefs, tribes and thinking, which are always accidents and never the essences of our humanity. We acquire them after getting out of the wombs of our mothers".
0 Comments