Naililia nchi yangu Tanzania. Sijaishi upande wa visiwani nikajua fika matatizo waliyonayo wenzetu hawa kuhusiana na mfumo wa utawala tulio nao. Ninachojua Zanzibar siyo koloni la Tanganyika. Natafakari, naona kama kuna kosa vile lilifanyika. Kama Tanganyika ilifutwa kutoa nafasi kwa nchi ya muungano inayoitwa Tanzania, kwanini pia tusifikilie kuondokana kabisa na hizi serikali ndani ya serikali!! Hivi Muungano huu ni wa nani? Kama si wa wachache, kwanini tusitangaze tu uwepo wa serikali moja ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania yenye kuongozwa na serikali moja na si mbili wala tatu!!. Tupeni basi nafasi tupige kura kama kusikilizana kwa kawaida imeshindikana. Hapo tutapata maoni sahihi ya kila upande. Hivi Tume ya Katiba kwanini wanapata kigugumizi kutoa pendekezo hili kama kweli muungano huu tunaupenda sote? SITAKI kufikia mahali kulazimika kuomba uraia wa Tanganyika au Zanzibari kama tokeo la shinikizo la mabadiliko toka kwa watu wachache wenye uchu wa madaraka!! Najaribu kutafakari!!!
Related Posts
- [wanabidii] Press Releases: Nicaragua's Independence Day
- [wanabidii] Press Releases: El Salvador's Independence Day
- [wanabidii] Press Releases: Presidential Determination for Major Drug Producing and Transit Countries
- [wanabidii] Africa: Counselor Thomas A. Shannon's Travel to Mogadishu, Somalia, on September 14
- [wanabidii] Press Releases: New U.S. Consulate General in Guangzhou, China Receives 2014 Green GOOD DESIGN(tm) Award
- [wanabidii] Press Releases: Papua New Guinea Independence Day
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Comments