[wanabidii] Kutoka Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya:Mfanyabiashara Mkazi wa ilolo Akamatwa akiwa na Kiungo cha Binadamu Sehemu ya Kiganja cha Mkono wa Kulia Nyumbani Kwake

Thursday, February 14, 2013
MNAMO TAREHE 12.02.2013 MAJIRA YA SAA 11:00HRS HUKO ENEO LA ILOLO JIJI NA MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WALIMKAMATA BARAKA S/O KIBONA,MIAKA 30,MNDALI,MFANYABIASHARA, MKAZI WA ILOLO AKIWA NA KIUNGO CHA BINADAMU SEHEMU YA KIGANJA CHA MKONO WA KULIA  NDANI YA NYUMBA YAKE .
 
MBINU ILIYOTUMIKA NI KUFICHA KIUNGO HICHO CHUMBANI NDANI YA BOX KWA KUZUNGUSHIWA KAMBA . MTUHUMIWA  ANAKIRI KUMILIKI  KIUNGO HICHO AMBACHO  ANADAI ALIPEWA NA MGANGA WAKE WA KIENYEJI KWA MADHUMUNI YA KUKITUMIA KIUNGO HICHO KWA AJILI YA  KUJIKINGA/KUJILINDA KATIKA BIASHARA ZAKE ZA KIMACHINGA ZISICHUKULIWE  KWA NJIA YA KISHIRIKINA IKIWA NI PAMOJA NA FEDHA ZAKE. 
 
TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE MAHAKAMANI. KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  MRAKIBU MWANDAMIZI WA POLISI BARAKAEL MASAKI ANATOA WITO JAMII KUACHA TABIA YA KUSADIKI IMANI ZA KISHIRIKINA  KWANI ZINA MADHARA MAKUBWA NA BADALA YAKE WAFANYE KAZI ZAO KWA BIDII KWA KUMCHA MWENYEZI MUNGU KUPITIA IMANI ZA DINI ZAO. 
AIDHA ANATOA RAI KWA JAMII KUENDELEA KUUCHUKIA UHALIFU KWA KUWAFICHUA WAHALIFU NA UHALIFU KATIKA MAMLAKA HUSIKA UNAOJITOKEZA KATIKA  MAENEO YAO.

      Signed by
[B.N.MASAKI -SSP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MBEYA
Kwa habari zaidi na picha:


http://goldentz.blogspot.com/2013/02/kutoka-jeshi-la-polisi-mkoani.html

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

Share this :

Related Posts

0 Comments