[wanabidii] HIVI JESHI LA POLISI NI KWA JILI YA CCM AU WATANZANIA WOTE?

Thursday, September 27, 2012
Naishangaa serikali na vyombo vyake vya dola hasa jeshi la polisi. Iweje wafanye mauaji ya kutisha na serikali isitoe tamko kwa waliohusika. Wao wakikamata kibaka wanampiga na kumburuza mahakamani  hadharani, lakini wao wakiua raia wanapelekwa mahakamani wakiwa wamefunikwa kama wanawali. Bandugu mnalionaje hili?
Walomuua Generali Kombe wako mtaani,
Walomuua Mwandishi wa habari iringa wako mtaani,
Walomtesa Dr. Ulimboka, wako mtaani;
Walotaka kumuua Highness na Mbunge wa Ukerewe, wako mtaani,
Kwa ujumla jeshi hili limekosa sifa za kuitwa la usalama wa  raia na mali zao badala yake ni kinyume.
Wewe Mwanabidii unalisemaje hili?
 
Mt. B;
Bukoba Municipal,
Tanzania - East Africa.

Share this :

Related Posts

0 Comments