[wanabidii] Press Releases: Randy Berry, Special Envoy for the Human Rights of LGBTI Persons, Travels to Latin America and the Caribbean

Sunday, May 31, 2015 Add Comment
[wanabidii] Press Releases: Randy Berry, Special Envoy for the Human Rights of LGBTI Persons, Travels to Latin America and the Caribbean

You are subscribed to Press Releases for U.S. Department of State. This information has recently been updated, and is now available.

05/31/2015 01:59 PM EDT

Randy Berry, Special Envoy for the Human Rights of LGBTI Persons, Travels to Latin America and the Caribbean


Media Note
Office of the Spokesperson
Washington, DC
May 31, 2015


Special Envoy for the Human Rights of LGBTI Persons Randy Berry will travel to Chile from June 1 – 2, Argentina from June 3 – 4, Uruguay from June 4 – 5, Brazil from June 6 – 9, and the Dominican Republic from June 10 – 11 to discuss the human rights of LGBTI persons and other historically marginalized groups.

During the 11 day visit, Special Envoy Berry will participate in LGBTI Pride Month activities and meet with government representatives, in addition to members of religious, business, academic, and civil society organizations.

For updates on the U.S. Government’s human rights work, visit www.humanrights.gov, the DRL Twitter account: @State_DRL or Special Envoy Berry’s Twitter account: @RandyBerry.

For more information, please contact DRL-Press@state.gov.


This email was sent to wanabidii@googlegroups.com using GovDelivery, on behalf of: U.S. Department of State · 2201 C Street NW · Washington, DC 20520 Powered by GovDelivery

[wanabidii] URAI 2015: Mapinduzi Kwenye Sekta ya Elimu!

Sunday, May 31, 2015 Add Comment
[wanabidii] URAI 2015: Mapinduzi Kwenye Sekta ya Elimu!

URAIS 2015: Mapinduzi Kwenye Sekta ya Elimu!

 

Kwenye awamu ya nne tumeshuhudia Serikali ya CCM ikijenga shule nyingi na kuzalisha na kuajiri walimu wengi kuliko kipindi chochote kile katika historia ya nchi yetu. Tumeshuhudia vyuo vingi vya elimu ya kati vikipanda hadhi na kuwa vya elimu ya juu, na tumeshuhudia idadi ya wahitimu wenye elimu ya chuo kikuu wakiongezeka mwaka hadi mwaka. Sambamba na jitihada hizi, tumeshuhudia wahitimu wakifanya usaili wa mchujo wa awali kwa ajili ya nafasi za kazi kwenye uwanja wa Taifa. Tumeshuhudia baadhi ya taasisi zikilalamikiwa kwa kutoa ajira kwa undugunaizesheni. Hii inatanabaisha kuwa tuna tatizo si tu la kukosa elimu yenye kutoa ujuzi wa kujiajiri bali pia tuna wasomi wengi wenye elimu ya juu kushinda mahitaji ya soko la ajira. Tumeshuhudia shule za kata zikitoa wahitimu wenye ubora ambao wamekuwa wakisonga mbele zaidi kwenye masomo yao, huku wengine wengi wakifeli . Ni lazima tufanye paradigm shift.

 

Ni wazi kwamba hatupaswi kuendelea kuwekeza kwenye kusomesha watu wetu kwenye elimu ya juu kwa kipindi hiki, pengine tujikite zaidi kuwekeza kwenye kuongeza ubora na kwenye utafiti na teknolojia.

 

Nini tunahitaji kwenye elimu sasa?

 

Tunahitaji:

 

(1.)         Kuongeza ubora wa shule zetu kwa kujenga maabara, maktaba, mabweni, viwanja vya michezo, karakana (zinapohitajika) na nyumba za walimu. Pia kuhakikisha shule zote nchini zinakuwa na umeme, maji na mtandao mzuri wa mawasiliano ili kuongeza ari ya walimu kuishi kwenye maeneo yote bila kuchagua (retention scheme).

 

(2.)         Kuboresha mitaala ili kuifanya elimu yetu iwape wanafunzi si tu elimu ya ufahamu bali pia ya ujuzi na uvumbuzi; na zaidi component ya elimu ya ujasiriamali na communication skills ni lazima.

 

(3.)         Tuanzishe mfumo wa motisha kwa walimu wetu kulingana na jiografia na mazingira wanapofanyia kazi (differential incentives scheme). Walimu wanaofundisha maeneo ya mbali na makao makuu ya wilaya na wanaofundisha kwenye maeneo yasiyo na huduma mbalimbali muhimu ni lazima walipwe posho maalum zaidi ya wenzao wanaofundisha maeneo ya mijini.

 

(4.)         Kuwa na mpango wa dharura wa kuanzisha shule za VETA kwa kuamua kuzigeuza baadhi ya shule za sekondari kuwa za VETA na kuziwezesha zipate vifaa na wakufunzi wenye ujuzi ili zianze mara moja kutoa mafunzo kwa vijana waliohitimu darasa la saba na hawakupata fursa ya kusonga mbele, na kwa wale waliohitimu kidato cha nne na hawakupata fursa ya kusonga mbele, na hivyo hivyo kwa waliohitimu kidato cha sita. Mpango huu utatoa fursa ya kupata vijana wengi wenye ujuzi kwa haraka kwa ajili ya kujenga vijiji na miji yetu (mafundi uashi, ubunifu wa mavazi, ushonaji nguo, useremala, mafundi bomba, umeme, madereva, mafundi mitambo, mabwana shamba vijijini n.k.). Shule za VETA zitatoa fursa kwa vijana waliopoteza matumaini, zitawapa ujuzi wa kujiajiri, lakini pia wahitimu wa VETA wanahitajika sana kwenye ajira za sekta binafsi.

 

(5.)         Kurekebisha mfumo wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa kuweka mfumo ambao unatoa usawa (equity) kwa mwanafunzi kulingana na hali ya uchumi wa familia yake na si kigezo cha kozi anayosoma pekee (mfano mwanafunzi mtoto wa mbunge ama wa waziri analipiwa gharama zote bure wakati mtoto wa maskini anayesomea biashara anatakiwa kujilipia aidha ada yote ama sehemu ya ada hiyo).

 

 

--
"Vision is the ability to see the invisible!"
Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA
P.O.Box 22499,
Dar es salaam.
Tanzania.
Phone No: +255 754 636963
                +255 782 636963
website: www.peercorpstrust.org or www.hamisikigwangalla.com
Email: hamisi.kigwangalla@peercorpstrust.org or info@hamisikigwangalla.com
Skype ID: hkigwangalla
Blog: blog.hamisikigwangalla.com 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

[wanabidii] HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WA KUTANGAZA NIA

Sunday, May 31, 2015 Add Comment
[wanabidii] HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WA KUTANGAZA NIA

HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WA KUTANGAZA NIA

UTANGULIZI:

Ndugu viongozi, wana-CCM na Watanzania wenzangu; Kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetufikisha hapa leo.  Lakini pia niwashukuru nyote mlioweza kufika hapa leo.  Kipekee niwashukuru  CCM wenzangu na Watanzania kiujumla ambao wameendelea kuwa marafiki na kuniuunga mkono. Hakika nimejawa na furaha.

Hii ni siku muhimu kwangu na kwa nchi yetu. Leo nimeamua kuwaita ili kuwatangazia rasmi azma yangu ya kuomba ridhaa ya chama chetu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili niteuliwe kukiwakilisha cha chetu kuwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Naamini historia itaihifadhi kama ni siku ambayo kwa mara ya pili katika maisha yangu, nimejitokeza kuwania kuiongoza nchi yetu kupitia chama chetu. Mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 1995 wakati wa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi hapa nchini nilipojitokeza nikiwa pamoja na Rais Jakaya Kikwete;

Wakati ule sote tulikuwa wanasiasa vijana. Pamoja tulikwenda kuchukua fomu na baadaye kwa pamoja tukazungumza na waandishi wa habari. Tulileta hamasa kubwa pale tulipofanya jambo ambalo halikuzoeleka kwa Watanzania kwa kutangaza kwamba yeyote atakayepita kati yetu, mwenzake ambaye hatafanikiwa angemuunga mkono.

Ningeweza kujitokeza tena mwaka 2005 lakini nikaamua kwa dhati kumuunga mkono Rais Jakaya Kikwete.

Nikiwa Mwenyekiti wa Kampeni niliwaongoza wenzangu kufanikisha ushindi mkubwa wa mgombea wetu, na baadaye ushindi mkubwa wa asilimia 80 kwa Chama Cha Mapinduzi kwenye uchaguzi mkuu wa 2005.

Nitaeleza kwa nini nimeamua kujitokeza tena, na kwa nini naamini mimi ndiye mtu sahihi wa kuiongoza nchi yetu wakati huu. Mpaka hapa itoshe tu kuwaeleza ni kwa nini naamini leo ni siku muhimu. Ni siku muhimu kwa sababu nina kiu ya kuona Watanzania wenzangu tunajiunga kuianza safari ya matumaini.

Ni siku muhimu kwa nchi yetu pia, kwa sababu naamini inajibu wito wa mahitaji ya sasa ya uongozi wa Taifa letu wa kumpata kiongozi imara atakayewaongoza Watanzania kujenga taifa imara. Na hili nitalieleza kwa kina. Hii ndiyo safari ya matumaini.

 

 

 

HALI YA NCHI NA MATARAJIO YA WATU:

Nchi yetu hivi sasa inapita katika kipindi kigumu, katika maeneo yote makuu ya kisiasa na kiuchumi.

Kisiasa, tumeshuhudia kuongezeka kwa vuguvugu la mfumo wa vyama vingi, ambapo ushindani kati ya vyama vya siasa unazidi kuwa mkali. Kwa bahati mbaya ushindani huo umefikia hatua ya kuchukua sura ya kuonekana kama vile ni mapambano ya watu binafsi badala ya kuwa mapambano ya sera na dira ya kuongoza nchi.

Tunashuhudia kuongezeka uhasama binafsi kati ya wanasiasa ndani ya chama kimoja kimoja, na pia kati ya wanasiasa wa chama kimoja dhidi ya kingine. Kadiri siku zinavyokwenda, hali inazidi kuzorota na ikiachiwa kuendelea nchi yetu inaweza kujikuta mahali pabaya.

Kukua kwa ushindani ni jambo jema linalokomaza na kurutubisha demokrasia yetu. Tukiwa na ushindani wenye afya unaweza kuwa chachu ya kuleta mabadiliko mema kwa wananchi, na kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika nchi yetu.

Tunahitaji uongozi imara katika kipindi hiki, ili kuondokana na siasa muflisi na kujenga siasa mpya zinazoimarisha ushindani wenye tija unaojikita katika kushindana katika kuwapatia huduma bora Watanzania. Hii ndiyo safari ya matumaini

Kiuchumi, tumeshuhudia ukuaji mzuri na kuongezeka kwa mapato ya ndani ya Serikali na uimarishaji wa mfumo wa uwajibikaji na ulipaji kodi. Kwa upande mwengine, Serikali ya Rais Benjamini Mkapa na Rais Jakaya Kikwete zimefanya kazi kubwa katika uendelezaji wa sekta ya mafuta na gesi asilia ambapo kiwango kikubwa cha gesi asilia kimegunduliwa. Tanzania sasa imekuwa ni miongoni mwa nchi zinazovutia uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo ambayo inatajwa kwamba inaweza kuja kubadilisha kabisa maisha ya Watanzania. Hata hivyo, kipindi hiki kuelekea ujenzi wa uchumi wa kisasa kimeshuhudia kuongezeka kwa hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi kwamba hawatonufaika na ukuaji huu wa uchumi na ugunduzi wa utajiri mkubwa wa gesi asilia.

Kwa upande mwingine, vijana wanataka kuona ukuaji wa uchumi na ugunduzi wa utajiri huo unakwenda sambamba na uzalishaji wa ajira zenye maana ili waweze kukabiliana na changamoto za maisha yao.

Niliwahi kusema kwamba tatizo la ukosefu wa ajira likiachiwa bila ya kutafutiwa ufumbuzi  ni bomu linalosubiri kulipuka. Vijana wasio na ajira hupoteza matumaini na ni rahisi kughilibiwa kuingiza nchi katika machafuko. Tunahitaji uongozi imara kuweza kuikabili hali hiyo na kuitafutia suluhisho maridhawa. Hii ndiyo safari ya matumaini

 

 

WATANZANIA WANATAKA MABADILIKO:

Ndugu zangu, mnaweza kujiuliza kwa nini nimeyaeleza yote hayo na yana mahusiano gani na dhamira yangu ya kutangaza nia ya kutaka kuiongoza nchi yetu kupitia CCM?

Watanzania wanataka mabadiliko yatakayowawezesha kukabiliana na changamoto hizi na kuwaongoza kujenga Taifa imara ambalo kila mwananchi wake anaishi akiwa na uhakika wa usalama wa maisha yake, mali zake na mahitaji yake muhimu. Papo hapo akijiridhisha kwamba leo yake ni bora kuliko jana yake, na kesho yake itakuwa bora zaidi kuliko leo yake. Kwa maneno mengine, Watanzania wanahitaji mabadiliko yatakayowapa uongozi imara, unaoweza kuwaongoza kujenga taifa imara. Hii ndio Safari ya Matumaini.

Naamini kwamba, hata katika kipindi hiki ambapo Watanzania wanataka mabadiliko, na wanaendelea kuamini kwamba CCM ina uwezo wa kusimamia mabadiliko hayo.

Lakini kama alivyotuusia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, mwaka 1995, wakati wa uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa vyama vingi hapa nchini, Watanzania wasipoyapata mabadiliko hayo ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM!

Sina shaka, CCM tunao uwezo wa kuwapa Watanzania mabadiliko wanayoyataka.

 

UONGOZI UNAOHITAJIKA KULETA MABADILIKO YANAYOTAKIWA:

Rais Jakaya Kikwete amefanya kazi kubwa katika kipindi chake na kama ambavyo amekuwa akisisitiza mara kwa mara katika hotuba zake za karibuni ni kwamba yeye ametekeleza wajibu wake. Pia amesema anamwachia atakayemkabidhi uongozi wa nchi yetu baada ya yeye kumaliza muda wake kuendeleza pale atakapoachia.

Kwa maoni yangu, ili kuifanya kazi hiyo na kuzikabili changamoto nilizozieleza, nchi yetu inahitaji uongozi wenye sifa zifuatazo:

      i)          Uongozi wenye uthubutu, usioogopa kufanya maamuzi magumu;

      ii)         Uongozi thabiti, makini na usioyumba;

      iii)        Uongozi wenye ubunifu na wenye upeo mkubwa;

      iv)        Uongozi unaoamini katika mfumo shirikishi katika ujenzi wa Taifa;

      v)         Uongozi unaozingatia muda katika kutekeleza majukumu yake.

 

Naamini pia kwamba wananchi wanataka Rais ajaye wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awe na sifa kuu zifuatazo:

1.      Aweze kuwaunganisha Watanzania

2.      Aweze kubuni sera na kusimamia utekelezaji wa mikakati ya kuinua uchumi wa Tanzania na kukuza pato la Mtanzania; ikiwemo kupunguza tofauti ya kipato kati ya aliyekuwanacho na wasiokuwanacho;

3.      Aweze kubuni sera na kusimamia utekelezaji wa mikakati ya kuzalisha ajira kwa vijana wetu;

4.      Awe kuwa mfano wa kuchapa kazi na kuwajibika;

5.      Aweze kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato na matumizi ya Serikali;

6.      Aweze kutumia fursa yetu ya kijiografia kibiashara.

7.      Aweze kusimamia matumizi ya raslimali zetu ili kuutokomeza umaskini wa Waatanzania

8.      Aweze kutokomeza mianya ya rushwa kwa vitendo;

 

UONGOZI IMARA, TAIFA IMARA:

Naamini kwamba uongozi wa juu wa nchi katika nafasi ya Urais si kazi ya lelemama, na unahitaji utashi. Kabla hata ya kushawishiwa na wenzako, ni lazima kwanza wewe mwenyewe uamini na uwaaminishe wenzio kwamba unao uwezo wa kuwaongoza wananchi wenzako.

Kuamini kama una uwezo na shauku, haina budi kwenda sambamba na uwezo wa kusimamia yale unayoyaamini. Na kwangu haya mwili ni dhahiri. Nina ari, nina shauku na nina uwezo, kama rekodi yangu inavyothibitisha.

Tunapomtafuta Rais wa Jamhuri ya Muungano ni lazima tukumbuke kwamba tunamtafuta mtu ambaye atakuwa pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama katika nchi yetu. Na kwa Chama Cha Mapinduzi tunamtafuta mtu ambaye atakuwa pia Mwenyekiti wa Chama chetu.

Naamini kwa vigezo vyote, nina kila sifa ya kubeba dhamana hizo nzito. Katika mambo ambayo najivunia, na sitoyasahau katika historia yangu ni kushiriki kwangu kuilinda nchi yetu pale ilipohitajika. Nilishiriki kikamilifu katika Vita vya Kagera nikiwa miongoni askari wa mstari wa mbele wa mapambano.

Kutokana na rekodi yangu inayoeleweka, naamini ninazo sifa za kuwaongoza Watanzania wenzangu katika zama mpya za ujenzi wa Taifa la kisasa, lenye watu wazalendo, walioshikamana na lenye uchumi imara unaomnufaisha kila Mtanzania. Naamini ninao uwezo wa kuwapa Watanzania Uongozi imara kwa ajili ya ujenzi wa Taifa Imara. Hii ndiyo safari ya matumaini

 

DIRA YANGU NA MATARAJIO YA WATANZANIA:

Najua kwamba Ilani ya CCM ya mwaka 2015 imo katika hatua za mwisho za kukamilishwa na itakapopata baraka za vikao vya Chama itakuwa ndiyo msingi wa utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano itakayochaguliwa Oktoba mwaka huu. Hata hivyo, naamini pia kwamba mgombea mwenyewe anayetaka ridhaa ya Chama na ya Watanzania kuongoza nchi naye anapaswa kueleza dira yake.

Baada ya kutafakari kwa kina changamoto tulizo nazo na matarajio na matumaini waliyo nayo Watanzania, naamini kwamba Uongozi imara unaolenga kujenga Taifa imara unapaswa kuwa na dira yenye malengo yafuatayo:

1.      Kuimarisha Muungano wetu kwa kuyashughulikia yanayotutenganisha na kuyafanyia kazi ili yasivuruge yale yanayotuunganisha ambayo ni mengi zaidi na makubwa zaidi.

2.      Kushughulikia matumizi mabaya ya siasa, za udini na ukabila na ubaguzi wa aina yoyote, kwa kuimarisha siasa zilizoshiba uzalendo na zenye kutuelekeza kwenye Utanzania wetu.

3.      Kujenga uchumi imara na wa kisasa, na ambao ni shirikishi unaomnufaisha kila Mtanzania aliyeko mjini au kijijini.

4.      Kuondokana na sifa mbaya ya kuwa Taifa ombaomba. Kwa wingi wa rasilimali tulizo nazo na neema ya ardhi, maziwa, mito na bahari, Tanzania tuna kila sababu ya kuacha kuwa 'bakuli la ombaomba' na badala yake kuwa 'mkoba wa neema' katika Afrika. "We can transform our nation from being the begging bowl to become the bread basket of Africa".

5.      Kujenga mfumo mpya wa elimu unaowatayarisha vijana wetu waweze kuajirika, kujiajiri na kushindana katika soko la ajira.

6.      Kuhakikisha ukuaji wa uchumi unenda  sambamba kuhakikisha haki, usawa na huduma za msingi za kila raia kama vile afya, maji safi nakadhalika.

Mambo haya niliyoyaeleza hapa ndiyo yatakayokuwa msingi mkuu wa utendaji wa Serikali nitakayoiongoza pale nitakapopewa ridhaa ya kubeba bendera ya CCM katika nafasi ya Urais na pia nitakapopewa ridhaa ya kuliongoza Taifa letu kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

 

RAMANI YA UONGOZI IMARA NINAOUAMINI (LEADERSHIP ROADMAP):

Kama nilivyotangulia kusema, kazi ya kuongoza nchi si lelemama na hasa unapoongozwa na dhamira ya dhati na msukumo wa ndani ya nafsi wa kubadilisha maisha ya wananchi wenzako waliokuamini uwaongoze. Kwa vyovyote vile, hiyo haiwezi kuwa kazi ya mtu mmoja. Ni kazi ya pamoja. Hata hivyo, Nahodha,  anayeongoza timu lazima awe na ramani itakayomuongoza, yaani 'Leadership Roadmap'.

 

Ndugu Watanzania, matatizo ya nchi yetu yanayotukabili sote tunayajua, kama nilivyoainisha hapo  awali.

Serikali za awamu zilizotangulia zimeyajadili na kujaribu kuyatafutia ufumbuzi. Mimi pia nimekuwa sehemu ya jitihada hizi wakati wa utumishi wangu katika chama na serikali huko nyuma.

Sasa mtauliza kama hii ndiyo hali halisi, ukiacha tu kuwa huu ni msimu mpya wa uchaguzi, kwa nini nagombea na ni kipi kipya?

Nimeamua kugombea urais ili kupambana na umaskini.  Ninapata hasira ninapoona umaskini ambao ungeweza kuepukwa kutokana na raslimali nyingi tulizonazo. Kinachohitajika hapa ni uongozi imara wa kutokomeza umaskini.

Ndugu Watanzania wenzangu, kama nilivyosema, Tanzania imepitisha sera na sheria nyingi na mipango mizuri. Tunayo Dira ya Maendeleo 'Vision 2025' ninaamini sera na sheria zinajitosheleza. Umuhimu si wingi au upya wa sera bali utayari na ubora wa utekelezaji wake.

Nia yangu ni kuimarisha na kusimamia utekelezaji wa sera zilizo bora na kurekebisha panapotakiwa ili kuchochea maendeleo ya watu yatakayosimamiwa na serikali inayojali.

Kipya ambacho uongozi wangu utaleta, ni mwanzo wa mchakamchaka wa maendeleo katika misingi ya utawala bora, na utendaji utajengwa katika nguzo zifuatazo:

1.      Kurejea kwenye Katiba katika kuainisha nia, dhamira na malengo yetu ya kujenga jamii inayozingatia misingi ya demokrasia, udugu na amani.

Muhimu katika hili ni kukemea na kuchukua hatua dhidi ya tabia mbaya, zinazochochea mfarakano katika jamii kama vile matumizi mabaya ya siasa za udini na ukabila.

Aidha moja ya misingi muhimu ya Katiba ni Muungano wetu. Itakuwa dhamira yangu kuimarisha misingi ya Muungano pamoja na udugu wa damu na historia ya ushirikiano iliyojengwa na waasisi wetu, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Sheikh Amri Abeid Karume na kuyaenzi Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

2.      Kujenga fikra mpya za kurejesha kujiamini na kufufua azma ya kujitegemea kama Taifa. Tuanze kwa kujipiga kifua kwa kujiamini kuwa tunaweza kujitegemea na kuijenga Tanzania sisi wenyewe. Kujiamini na kujitegemea ndio uhuru wa kweli.

 

3.      Kujenga uzalendo, uadilifu ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwazi katika shughuli zote za serikali na kupambana na rushwa. Tukumbuke kuwa hatuwezi kujenga uchumi wa kisasa kama tutaruhusu rushwa ishamiri. Wawekezaji hawataleta mitaji yao kwa wingi kama rushwa itaendelea kutawala katika huduma serikali na wananchi hawawezi kupata huduma bora kama rushwa itaendelea kutawala. Ni lazima tuipinge rushwa kwa vitendo sio maneno.

 

 

4.      Kujenga Serikali madhubuti, makini na yenye nidhamu inayoendeshwa kwa misingi ya sheria, uwazi na uwajibikaji. Maendeleo ya watu hayawezekani bila serikali kusimamia utekelezaji sera na miradi na kuleta ufanisi katika kutoa huduma na kusimamia maendeleo. Tumekuwa wepesi wa kutunga sera lakini wazito wa kuzitekeleza na kuzisimamia.

 

5.      Kuleta msukumo mpya wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi wa kisasa na unaojitegemea. Sekta binafsi ndiyo nyenzo ya uchumi imara. Inazalisha mali, ajira na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa kwa kulipa kodi. Ili sekta hii itoe mchango unaotakiwa katika maendeleo ni lazima ifanye kazi na serikali kwa karibu. Tukumbuke, bila uchumi imara hakuna huduma bora!

 

 

6.      Uwekezaji katika huduma za jamii. Elimu na afya bora, michezo, mazingira, makazi safi na maji salama ndiyo mihimili ya maendeleo ya watu. Hii inawezekana tu iwapo serikali itakuwa na sera na utashi wa kuutambua uboreshaji wa huduma za jamii kama ndiyo lengo kuu la maendeleo ya nchi. Napenda kusisitiza kuwa, elimu ndiyo muhimili wa maendeleo, ndiyo mkombozi wa kweli wa binadamu. Mimi ni mfano hai wa ukombozi wa elimu. Elimu ndiyo imenivusha kutoka kijijini kwetu Ngarash na kunipa upeo wa kitaifa. Mama akiwa na elimu atatambua umuhimu wa kumpeleka mwanae shule, anapata lishe bora na chanjo stahili na kuwa anaishi katika mazingira safi. Mkulima akipata elimu stahiki, atakuwa mkulima bora na kilimo chake kitampa tija na kumletea maendeleo. Elimu ndilo silaha dhidi ya umaskini, maradhi na ujinga.

 

7.      Kujenga uchumi shirikishi unaolenga kuondoa umaskini. Mkakati wa kuondoa umaskini Tanzania lazima ujikite kwenye nguzo za ushiriki wa kila Mtanzania katika uchumi wa taifa. Kwa misingi hii, tukiweza kupunguza umaskini, tutaweza pia kupunguza ukubwa wa tofauti za kipato kati ya walio nacho na wasionacho, ambazo tukiziacha ziendelee kukua kwa kiasi cha sasa, zinawezakuhatarisha utulivu na amani katika jamii yetu. Uchumi shirikishi ndio silaha dhidi ya umaskini.

 

8.      Kuimarisha ulinzi wa nchi na usalama wa raia na ujirani mwema. Itakuwa nia yangu kuimarisha misingi iliyojengwa kulinda na kudumisha umoja na amani nchini. Kadhalika, nitahakikisha kuwa usalama wa mipaka ya Tanzania unaimarishwa kwa misingi ya ujirani mwema na kutanzua migogoro na matatatizo yoyote na nchi jirani, kwa njia ya diplomasia na mazungumzo.

 

HITIMISHO:

Hii ndiyo misingi na dira ya uongozi wangu. Nachelea kusema kuwa haitakuwa kazi rahisi. Lakini kwa ushirikiano wa kila mmoja na kufanya maamuzi magumu, yote yanawezekana. Tumeona nchi nyingi zilizosimamiwa na utawala thabiti wa serikali za kimaendeleo zikikabili na kupunguza umaskini katika kizazi kimoja. Kama mataifa mengine yamefanikiwa, tena bila ya kuwa na raslimali kama zetu, kwa nini sisi tushindwe?

Napenda kumalizia kwa kusisitiza yafuatayo:

1.      Tutahakikisha kuwa tunajenga uchumi imara ikiwa ni pamoja na kujenga viwanda na kukuza utalii, kuboresha kilimo, uvuvi, mifugo na kuhakikisha kuwa tunasarifisha mali ghafi badala ya kuuza mazao yetu nje.

2.      Tutahakikisha kuwa rasilimali za nchi ikiwa pamoja na gesi asilia zitatumika kwa manufaa ya kila mwananchi kwa lengo la, kuondoa umasikini

3.      Tutahakikisha kuwa tutakabiliana na rushwa kwa vitendo na si kwa maneno, na kuimarisha mshikamano wa taifa

4.      Tutahakikisha tutaanza safari ya matumaini ya kuwapatia Wanzania elimu bora itakayoleta mapinduzi ya fikra.

5.      Tutahakikisha tunaboresha maslahi ya walimu na ya wafanyakazi wengine wa sekta ya umma.

6.      Tutaanza mchakato wa kuwapa watanzania matumaini mapya ya kujiwekea akiba na kunufaika na mifuko ya hifadhi ya kijamii

7.      Tutahakikisha kuwa Watanzania wote wanapata huduma bora za afya, maji safi na salama

8.      Tutahakikisha tunakabiliana na kutatua tatizo la ukosefu wa kazi kwa kubuni na kuongeza vyanzo vya ajira

9.      Tutahakikisha kuwa wafanya biashara wadogo wadogo na sekta isiyo rasmi, kwa kama vile wamachinga, bodaboda na mama ntilie watawekewa utaratibu bora zaidi wa kufanya na kuendeleza shughuli zao

10.  Tumechoka kuwa kichwa cha mwendawzimu katika michezo na washiriki washindwa.

11.  Tutatengeneza mazingira mazuri ya kuwezesha Watanzania waishio nje kuchangia kujenga na kukuza uchumi wa nchi yetu

12.  Tutaboresha miundo mbinu ili kukabiliana na adha ya msongamano katika jiji la Dar Es Salaam, Arusha, Mwanza na Mbeya; ni lazima tulivalie njuga jambo hili kuhakikisha linatatuliwa kwa haraka sana.

 

Ndugu Watanzania:-

Ni maono yangu kuwa siku si nyingi, nchi yetu itaanza safari yenye uelekeo wa matumaini na neema tele kwa wananchi.

Ni maono yangu kuwa siku si nyingi sisi kama Watanzania, kwa umoja wetu tutajivunia kuishi katika nchi tunayoipenda na inayoendeshwa kwa misingi ya utawala bora, chini ya serikali ya kimaendeleo iliyojengwa kwenye fikra mpya za uzalendo, uadilifu, utendaji na uwajibikaji.

Ni maono yangu, siku si nyingi Watanzania watajikwamua kutoka katika janga la umaskini na kwamba taifa letu litakuwa na uchumi imara na hatimaye kujitegemea.

 

Mimi si mtu ninayeamini kuongoza taifa ambalo watu wake wanajivunia umaskini.

Huwezi ukawa kiongozi ya nchi maskini, unayelenga kupunguza umaskini halafu ukawa unashabikia umaskini na kuuona ni sifa ya taifa.

Tuna kila sababu ya kufanya maamuzi magumu sasa ili kuwajengea Watanzania matumaini mapya ya maendeleo. Tuanze pamoja mchakamchaka wa amendeleo

Watanzania wenzangu, peke yangu sitaweza, lakini kwa maamuzi magumu na ushirikiano wa wananchi wenzangu, inawezekana kuanza safari ya matumaini mapya.

Naomba nihitimishe kwa kuwaomba wana CCM ikiwa ni pamoja na wagombea wenzangu, waniunge mkono na tujumuike kwa pamoja katika safari hii ya matumaini.

Safari tuianze leo, hatuna kesho nyingine.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa

 

Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

[wanabidii] Watch the Parade - Live, Kerry breaks a leg, No Mass at King David's Tomb - May 31, 2015

Sunday, May 31, 2015 Add Comment
[wanabidii] Watch the Parade - Live, Kerry breaks a leg, No Mass at King David's Tomb  - May 31, 2015

Email look weird? View it on the web here .

May 31, 2015 / 13 Sivan 5775

Cartoons


 

Headlines & Recommended

WATCH LIVE: New York Celebrates the Israel Day Parade [live video]
New York celebrates one of its largest, most popular parades of the year, starting at 11 am (NY time): the Israel Day Parade.
Nefesh B'Nefesh marches in the 2013 Israel Day Parade.


Protesters Prevent Mass in King David's Tomb
Hundreds of Jews barricaded themselves inside the lower hall of King David's tomb on Mount Zion on Sunday morning to prevent a Christian Mass ceremony in the Jewish prayer hall.
Orthodox Jew at King David's Tomb in Old City of Jerusalem.


Obama's Legacy: Many New Jewish Republicans
During Obama's tenure, Jews identifying as Republican or "leaning" Republican jumped more than 50%
President Barack Obama


Social Security Administration Paid $20 Million to Nazi Suspects
Thousands of former Nazi war criminals lied their way into the United States and later received old-age benefits.
Social Security payments were offered to Nazi criminals who agreed to leave the United States voluntarily/


PFLP Terrorists Condemn Rajoub for 'Wasting Blood of Martyrs'
FIFA's Palestinian Authority soccer chief dropped the ball on his own head.
PA's soccer chief Jibril Rajoub, a member of the Fatah Central Committee.


Jailed Terrorist Uses Smuggled Cell Phone for Gaza Radio Interview
Israel prison officials are investigating the security slip.
Abdallah Barghouti.


Helsinki Environmental 'World Village' Bans Jewish National Fund
The festival also blocked a Freedom of Speech Village that was to include an "I am Charlie" exhibition.
BDS poster in a campaign that charges the Jewish National Fund planting trees as a cover for


Why All the Racism and Bigotry When a Jew Buys a House?
The problem isn't Jews legally buying homes, it's Israel's neighbors denying Israel's right to exist
Philanthropists Cherna and Irving Moskowitz (on left)


Jeb Bush Vows to Move US Embassy from Tel Aviv to Jerusalem
Does he actually mean that moving the embassy will not endanger America's national security?
Jeb Bush.


Read more Headlines & Recommended articles
 



Click for your Print subscription to The Jewish Press .


Forward this email to a friend .

Received this from a friend? Subscribe .

We hope you won't, but if you must, you can unsubscribe instantly from these emails by clicking here.