[wanabidii] UJUMBE WANGU KWA SIKU YA UKIMWI DUNIANI 2013

Saturday, November 30, 2013 Add Comment
[wanabidii] UJUMBE WANGU KWA SIKU YA UKIMWI DUNIANI 2013

UJUMBE WANGU KWA SIKU YA UKIMWI DUNIANI  2013


Ndugu zangu ,


Kesho ni siku ya ukimwi duniani , kwa wanaofuatilia vyombo vya habari watakuwa wameshapata habari za hapa na pale kuhusu siku hiyo .


Kwa upande wangu wapenda kuwasihi watu haswa vijana wenzangu kujenga utaratibu wa kuangalia afya zao ili kujijua kabla ya kufanya baadhi ya maamuzi ambayo wanaweza kujutia katika maisha yao au kwa watu wengine ambao wanaweza kuathirika kutokana na mmoja kupata maambukizi .


Sio kweli kwamba kila muathirika ameambukizwa kutokana na kushiriki ngono ambazo sio salama , wengine wanafanya ngono salama na wapenzi wao au wanandoa wenzao na wanaambukizana wengine ni kwenye shuguli zao za kila siku kama mahospitalini wengine kwenye ajali .


Pamoja na kuathirika naamini kila mmoja katika jamii kwa kutumia nafasi yake au fursa aliyonayo anauwezo wa kupunguza maambukizi au kushinda vita hii katika maisha yake .


Kwa wale wafanyakazi wajue waajiri wao bado wanawapenda bado wanahitaji mchango wao katika shirika au kampuni husika .


Kwa wale kina baba au mama wajue bado wanahitajika kutunza familia zao haswa watoto wao waliowazaa wenyewe , wajipe muda kuongea na watoto wao kuhusu suala hili .


Kwa wafanyabiashara wajue serikali inahitaji kodi yao kutokana na biashara zao , watu wanahitaji ajira kwa wingi , unapoumwa au kufariki mapema basi ndoto nyingi zinapotea .


Kwa wanafunzi wajue wanahitajika kusoma kwa jitihada ili wawe kwenye kundi bora kati ya hayo hapo juu .


Kwa waathirika wasikate tamaa wanaweza kuendelea kutumia dawa na kufuata ushauri wa madaktari wataweza kuishi muda mrefu zaidi .


Kwa walimu wajue wao ndo wazalishaji wa wote hapo juu , wafanyakazi , wafanyabiashara , wanafunzi  , viopngozi na watu wa aina mbalimbali tunategemea wao wawe na maono zaidi kuhsu suala hili .


Kwa wengine wote , poleni kwa kupoteza ndugu , marafiki na majamaa kutokana na janga hili – tafadhali tuendelee kutoa elimu zaidi , tuendelee kuvumiliana na tuendelee kujenga taifa letu .

 

YONA FARES MARO

0786 806028 


--
Find Jobs in Africa Jobs in Africa
International Job Opportunities International Job Opportunities
Jobs in Kenya Jobs in Kenya

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[Mabadiliko] Mtoto Mtanzania ashinda insha EAC

Saturday, November 30, 2013 Add Comment

Peter Robert Kilave, mwanafunzi wa kidato cha tatu wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Tushikamane ya mjini Morogoro, amechukua ushindi wa kwanza kwa wanafunzi wote wa shule za sekondari wa nchi tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika shindano la insha kuhusu ujenzi wa miundombinu Afrika Mashariki. 

Amepewa tuzo ya dola za Marekani 1,500 na cheti na Mwenyekiti mpya wa Jumuiya, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya. 

Hiyo ilikuwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa EAC jijini Kampala, leo Jumamosi, Novemba 30, 2013. Rais Jakaya Kikwete alimwita jukwaani na kumpa mkono wa pongezi huku ukumbi ukizizima kwa shangwe. 

Kijana huyo mtanashati na mpole alijizolea dola zingine kutoka kwa viongozi na maafisa wa Serikali ya Tanzania kwa kuibeba Tanzania katika kipindi hiki chenye changamoto za ajabu ajabu ndani ya Jumuiya.

Mshindi wa pili alitoka Uganda; wa tatu Burundi; wa nne Rwanda na Mkenya alishika mkia. 

Dogo huyo wa Tanzania ataendelea kuvinjari nchini Uganda kwa siku ili wamwone kwa karibu zaidi. Atakuwa na maafisa wa EAC, afisa mwandamizi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Tanzania pamoja na mwalimu mkuu wake.

Hongera Watanzania wote.


Matinyi.


From my Android phone on T-Mobile. The first nationwide 4G network.

[wanabidii] Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Monduli asimamishwa

Saturday, November 30, 2013 Add Comment
[wanabidii] Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Monduli asimamishwa
TAARIFA KWA UMMA

Kwa niaba ya baraza la uongozi la mkoa wa Arusha, napenda kuujulisha umma wote kwa ujumla kuwa mwenyekiti wa wilaya ya monduli Mchungaji Amani Silanga Mollel amekoma/amesimamishwa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya monduli kuanzia tarehe 29 Novemba 2013 kufuatia tuhuma nzito za uvunjifu wa kanuni za maadili ya chama. 

Hatua hii imefikiwa baada ya kuthibitika na yeyé mwenyewe kukiri mbele ya kikao cha kamati tendaji ya wilaya ya monduli kilichoketi tarehe 29 Novemba 2913 saa NNE asubuhi kuwa alitoa tamko batili akitumia wadhifa wa mwenyekiti wa wilaya bila ridhaa ya kamati tendaji na huku akidanganya kuwa ni tamko kwa niaba ya wilaya ya monduli. 

Katika tamko lake ametoa tuhuma dhidi ya wajumbe wa kamati kuu na viongozi wakuu wa kitaifa kwa maamuzi halali ya kikao cha kamati kuu huku akijua kuwa anavunja kanuni za chama kwa mujibu wa katiba ya chama toleo la mwaka 2006 ya Kanuni za uendeshaji kazi za chama, sura ya KUMI, ibara ya 10 (X) "Kiongozi asitoe tuhuma zozote juu ya viongozi wenzake pasipo kupitia vikao halali na kuzingatia taratibu na ngazi zilizoelezwa kwenye kanuni za chama". 

Sambamba na hilo, Mchungaji Amani Silanga ametoa tuhuma za uzushi, uongo na upotoshaji na kutaka kuaminisha jamii kuwa chadema ina makundi ya CHADEMA Asili na CHADEMA Family kitu ambacho ni upotoshaji mkubwa na wa hatari kwa ustawi na umoja wa chama na kinyume na kanuni za uendeshaji kazi za chama, sura ya KUMI, ibara ya 10 (VII), "Kiongozi anatakiwa kuwa mkweli na muwazi wakati wote hususani katika vikao halali na aachane na vikundi vya majungu, wadanganyifu (Rumour Mongers). 

Ni mwiko kwa kiongozi kujihusisha na upotoshaji wa maamuzi wa vikao halali". Kamati tendaji ya wilaya ilipomtaka aonyeshe CHADEMA asili ni kina nani na CHADEMA family ni kina nani alishindwa kutoa maelezo yoyote ya maana na kufikia hatua ya kutaka kuvuruga kikao kwa kuleta vijana wahuni wapatao 17 ndani ya kikao ambao wengi walijulikana kuwa sio WANACHADEMA.

 Katika utambulisho wake wa majigambo Mchungaji Amani SIlanga kwa kiburi na kejeli amejitambulisha na kukiri kuwa yeye yupo kambi ya Zito Kabwe na hakuna wa kumfanya kitu maana ni mjumbe wa baraza kuu la chama. Maneno yake yalidhihirisha kuwa Mchungaji Amani Silanga anashiriki mpango wa kuunda makundi yasiyo na tija ndani ya chama na hivyo kuwa kinyume na sura hiyo hiyo ya kumi ya kanuni za uendeshaji kazi za chama ibara ya 10 (IX), "Kiongozi asijihusishe au kushiriki na vikundi au vitendo vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya uongozi wa chama au wanachama wake".

AZIMIO LA BARAZA LA UONGOZI LA MKOA WA ARUSHA:

Baraza la uongozi la mkoa lililoketi tarehe 29 Novemba 2013, limepokea mapendekezo ya kamati tendaji ya wilaya na kuzingatia hofu kubwa iliyoainishwa na kamati tendaji kufuatia matendo mengi yanayotia shaka ya uadilifu na uwezo wa kiuongozi wa Mchungaji Amani Silanga na hivyo baraza la uongozi la mkoa limeridhia kuwa amevunja kanuni za maadili ya chama sura ya KUMI ibara ya (VII) hadi (XII) na hivyo kupelekea ukomo wa yeye kuwa Mwenyekiti wa wilaya kuanzia tarehe 29 Novemba 2013. Baraza la mkoa likiwa mamlaka ya nidhamu kwa mujibu wa katiba ibara ya 6.3.6 (a) (iv) limemjulisha tuhuma zake na hatua hii stahiki iliyochukuliwa. 

Kwa vile Mchungaji Amani Silanga alikiri kosa hili mbele ya kamati tendaji ya wilaya bila kulijutia au kuomba msamaha, baraza la mkoa limechukua hatua hii stahiki kwa maslahi ya chama na kuwa uchunguzi zaidi utafanyika ili kufikia maamuzi makubwa zaidi ya tuhuma nyingi kwa mujibu wa kanuni za hatua za kinidhamu.

Baraza la uongozi la mkoa wa Arusha, linatoa onyo kwa wote ambao wapo katika mtandao huu mchafu, ama watoke wenyewe mapema maana hawatavumiliwa kamwe. Baraza la uongozi wa mkoa liliona kuwa Mchungaji Silanga amepotoka na hivyo yeyé kuendelea kuwepo ndani ya chama wakati wa uchunguzi wa tuhuma hizi nzito dhidi yake ni hatari zaidi kwa ustawi wa chama na hivyo baraza likaridhia kwa kuzingatia tafsiri ya katiba ya chama ibara ya 6.3.4 (c) wa yeyé kukoma uongozi na hivyo akae nje kwa muda na waliopotoka wenzake.


Amani Golugwa
Katibu wa CHADEMA – Mkoa wa Arusha.
(Kwa niaba ya Baraza la Uongozi la Mkoa wa Arusha)
Tarehe 30 Novemba 2013

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[wanabidii] MIKOA SABA KUNUFAIKA NA MPANGO WA KUINUA UBORA WA ELIMU NCHINI

Saturday, November 30, 2013 Add Comment
[wanabidii] MIKOA SABA  KUNUFAIKA NA MPANGO WA KUINUA UBORA WA ELIMU NCHINI

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

TAARIFA KWA UMMA
Novemba 29, 2013
MIKOA SABA  KUNUFAIKA NA MPANGO WA KUINUA UBORA WA ELIMU NCHINI  


Katika kuinua ubora wa elimu nchini, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza kupitia shirika lake la Department for International Development (DfID) itaanza kutekeleza Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu nchini [The Education Quality Improvement Programme in Tanzania (EQUIP – Tanzania)] kuanzia mwaka ujao, 2014.

Mikoa itakayonufaikia na mpango huu wa miaka minne (4) katika awamu ya kwanza kuanzia mwaka 2014 ni Dodoma, Kigoma, Shinyanga, Simiyu na Tabora. Awamu ya pili itaanza mwaka 2015 na kuhusisha mikoa ya Mara na Lindi.  

Mpango huu una lengo la kuinua ubora wa elimu ya msingi na kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari hasa wasichana. Aidha, mpango huu  utanufaisha wilaya 36 zenye shule za msingi zaidi ya 4,000 za serikali katika 
mikoa hiyo ambao utasimamiwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na TAMISEMI.

Akizungumzia utekelezaji wa Mpango huu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome  amesema kuwa mpango huu utasaidia kuinua kiwango cha ubora wa elimu katika mikoa husika.

'Tunaanza na mikoa hii ambayo baadhi yake imekuwa ikifanya vibaya katika matokeo ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi ili kuhakisha kuwa ubora wa elimu unaimarika na hatimaye kuongeza ufaulu wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari,'  anasema Profesa Mchome.

Mpango huu wa Kuinua Ubora wa Elimu utatoa mafunzo kazini kwa walimu kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kitaalam na kuongeza ufanisi katika kufundisha na kujifunza, kuimarisha mbinu za usimamizi na uendeshaji wa shule, kuimarisha mifumo itakayosaidia usimamizi wa elimu katika wilaya na mikoa, kuimarisha ushiriki wa jamii na kuhimiza uwajibikaji  katika masuala ya elimu.

Ni matumaini ya Wizara kuwa wadau wote katika Mikoa na Wilaya husika watatoa ushirikiano wa kutosha katika utekelezaji wa mpango huu. Lengo ni kupata Matokeo Makubwa Sasa.

Ntambi Bunyazu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[wanabidii] Taarifa ya Mabadiliko katika Jeshi la Polisi Tanzania

Saturday, November 30, 2013 Add Comment
[wanabidii] Taarifa ya Mabadiliko katika Jeshi la Polisi Tanzania
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema   amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera pamoja na baadhi ya Wakuu wa Upelelezi wa mikoa na  wakuu wa Polisi wa Wilaya katika baadhi ya mikoa hapa Nchini. 

Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Philipo Kalangi amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam, kuwa Mkuu  wa kikosi cha kusimamia usalama wa Mazingira na nafasi yake  inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) George Mayunga ambaye alikuwa Mkuu wa kikosi cha  kusimamia mazingira Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.

 Aidha, baadhi ya Wakuu wa Upelelezi wa  mikoa (RCO) na wakuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) waliobadilishwa ni pamoja na 
aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa  makosa ya jinai mkoa wa Tabora ACP Edward Bukombe amehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam, Mkuu wa Upelelezi wa mkoa wa Geita (RCO) ACP Francis Kibona  amehamishiwa mkoa wa Njombe kuwa mkuu wa Upelelezi mkoa na  nafasi yake inachukuliwa na SSP Simon Pasua kutoka  Makao makuu ya Upelelezi Dar es Salaam.

Wengine ni aliyekuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ya Wanging'ombe SSP. Francis Maro amehamishiwa Mkoa wa Katavi kuwa Mkuu wa upelelezi wa mkoa na aliyekuwa mkuu wa upelelezi mkoa wa Katavi ACP. Emmanuel Nley amehamishiwa kikosi cha Polisi wanamaji Dar es Salaam. Mkuu wa Upelelezi mkoa wa  Rukwa SSP. Peter Ngussa amehamishiwa Makao makuu ya Upelelezi Dar es Salaam, nafasi yake inachukuliwa na SSP  Alan Bukumbi aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Njombe.

Aliyekuwa Mkuu wa Polisi wilaya ya kati( OCD) Mrakibu wa  Polisi (SP) Salum Ndalama anaenda kuwa kaimu mkuu wa upelelezi mkoa wa Tabora na aliyekuwa mkuu wa Polisi wa  wilaya ya Tunduru (OCD) SP. Amadeus Tesha anakwenda kuwa Mkuu wa upelelezi kikosi cha Polisi reli.  

Uhamisho huo ni wa kawaida katika kuboresha utendaji kwa  mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi. 

Imetolewa na: 
Advera Senso-SSP 
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[wanabidii] TAARIFA YA KUJIUZURU KWA MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA LINDI

Saturday, November 30, 2013 Add Comment
[wanabidii] TAARIFA YA KUJIUZURU KWA MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA LINDI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI YA NDUGU ALLY O. CHITANDA

NDG: WANA HABARI:
Kwanza kabisa ninawashukuru kwa kuitika wito wangu. 

Jina langu naitwa ALLY OMARY CHITANDA, nimejiunga CHADEMA mwaka 2003 nikitokea NCCR –MAGEUZI.

Nyadhifa nilizowahi kuzishika na kukitumikia Chama ni:-

Kuanzia mwaka 2004- Mjumbe wa Baraza kuu Taifa nikiwakilisha vijana Bara niliendelea kuaminiwa na Chama na kupewa kazi nyingine za kukitumikia Chama, nimewahi kuwa Afisa wa Vijana Makao Makuu, Afisa wa sheria na Haki za binadamu Makao Makuu, Katibu wa Kamati ya muda ya Baraza la Vijana Taifa (BAVICHA) kwa sasa ni Mjumbe wa Mkutano Taifa nawakilisha Nachingwea, Mwenyekiti wa Mkoa wa Lindi tangu tarehe 26/05/2013.Pia ni Afisa Mwandamizi Ofisi ya Katibu Mkuu Makao makuu Dsm.

vile vile kwa kipindi kirefu sasa nimekuwa nikifanya shuhuli ya uandishi wa kumbukumbu za sekretarieti ya chama kama KATIBU WA SEKRETARIETI YA KAMATI KUU.
Hivyo sasa, pamoja na mambo mengine yapo masuala nyeti na muhimu ninayoyafahamu na ikibidi kuwaarifu watanzania kwa njia mbali mbali pindi itakaponihitaji kufanya hivyo.

Ndugu zangu wanahabari, nimewaita ili kupitia nyinyi niwaambie Watanzania wenzaqngu juu ya hali ya kisiasa ilivyo hasa ndani ya Chama chetu. Itakumbukwa kuwa tarehe 20-21/11/2013 Kamati kuu ya Chama ilikaa pamoja na mambo mengine ilifanya maazimio ya kuwavua nafasi za Uongozi ndani ya Chama alikuwa Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara Mhe. ZITTO KABWE na Mjumbe wa Kamati kuu wa kuchaguliwa Mhe. Dr. FITILA MKUMBO, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa sababu:-

(a) Mhe. ZITTO KABWE (Mb) alishiriki kusaidia Wabunge watatu wa CCM kupita bila kupingwa kenye Majimbo yao ya Uchaguzi 2010.

(b) Kuandaa mkakati waliouita mabadiliko ya Chama 2013. Mkakati uliolenga kumuwezesha Mhe. Zitto kushinda nafasi ya Uenyekiti wa Chama Taifa endapo angekubali kugombea.

(c) Mhe. Zitto alishindwa kutimiza majukumu yake ndani ya Chama kwa kutoshiriki pamoja na Viongozi wenzake kwenye matukio makubwa yaliyokikumba Chama kama:-
(i) Maandamano ya Arusha.
(ii) Operesheni zilzofanyika Morogoro na Iringa nk.

MAAMUZI MENGINE YA UBORESHAJI WA MAKAO:
Ni kweli kuwa pamoja na mambo mengine Baraza kuu la Chama iliridhia pendekezo lililetwa kwake na Kamati Kuu kuhusu jambo hili.Na katika utekelezaji wake Kamati Kuu ya juzi iliridhia kuwa, uteuzi wa Wakurugenzi watano ambao ni:-
1. Mkurugenzi wa Oganaizesheni Mhe. Singo Kigaila Benson.
2. Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano ya ndani Mhe. John Mnyika (Mb).
3. Mkurugenzi wa Fedha na uwekezaji Mhe. Anthony Komu.
4. Mkurugenzi wa Bunge na Halmashuri Mhe. John Mrema.
5. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama Mhe. Wilfred Lwakatale.

Uteuzi huu hauonyeshi sura ya Kitaifa Wakurugenzi wote watano ni Wakristo kanakwamba CHADEMA hakuna Waislamu wenye uwezo wa kushika nafasi hizo.

Lakini pia hauzingatii mgawanyo wa kijamii kwa kuwa kati ya kurugenzi hizo sita wakurugenzi wanne kati yao wanatokea mkoa mmoja wa kilimanjaro

Na uteuzi huu unakwenda sambamba na kuboresha maslahi yao kwa kuongeza posho, -kutoka Tshs. 800,000/= za awali na sasa itakuwa ni kuanzia Tshs. 1,500,000-2,500,000/= kwa Mkurugenzi na kutoka Tshs. 6,800,000/= kwa Afisa Mwandamizi na sasa ni Tshs.1,000,000-1,500,000/=.

Pamoja na kwamba uboreshaji uliridhiwa, lakini katika mpango ulioridhiwa na Baraza kuu ni pamoja na kulipa Posho kwa Makatibu wa Wilaya na Mikoa. Hawa ndio watendaji muhimu katika Ujenzi na Uhai wa Taasisi hii lakini, hawakuangaliwa wala kuguswa badala yake wanatakiwa kujitolea tu kwa hali na mali.

Mimi kama nilivyotangulia kusema hapo awali, kuwa niko kwa kwa miaka 10 sasa na nimeshiriki kwa kiasi kikubwa katika Ujenzi wa Chama hiki.Sioni sababu ya kutoharakisha kulipa posho ya Mkatibu wa Wilya na Mikoa pamoja na watendaji wengine na badala yake tunaharakisha kujilipa posho nono sisi watendaji wa Makao Makuu, wakati hawa wa ngazi za chini wanamaeneo makubwa ya Kiutendaji na wanafanya kazi katika mazingira magumu kwa kujitolea hata Ofisi zao wanajitolea wenyewe.

MAAMUZI YA KAMATI KUU
Ningependa kuwaambia wanachadema na watanzania kwa ujumla, maamuzi haya ya kamati kuu ya kuwavua uongozi zitto kabwe na dkt mkumbo ni maamuzi ya kijuha na yanayowafanya watanzania sasa waangalie mara mbili mbili kama hawa watu wapo makini na huo ukombozi wanaousema.

Tumekuwa tukiweka mikakati mbali mbali ya ushindi ili chama kishinde, kwa mfano, kabla hata ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa arumeru mashariki, wakati tu ilipobainika anaugua, chama kiliandaa mkakati wa kushinda ubunge wa jimbo hilo na uchaguzi uliporudiwa mkakati ule ulitumika na kushinda.

Nikiwa mtendaji wa ofisi ya katibu mkuu, nimeshiriki pamoja na zitto kabwe na dkt Slaa kupanga mikakati mbali mbali mizuri na mibaya kwa nchi, lakini hatukuwahi kuitwa wasaliti, wahaini wala sina lolote baya. Ni fedheha leo mimi kuwa sehemu ya watu wanaomuita zitto kabwe ni msaliti. Siwezi kuendelea na ujinga huu na sipo tayari tena.

Si dhambi kumuhukumu mtu kwa kuwa anapanga mipango ya kukushinda kwenye uchaguzi, dawa ya mpinzani wako ni kumkabili.

Naomba nikiri kwamba nikiwa katibu wa sekretarieti tumekuwa tukilazimishwa mara kadhaa kuwashawishi wajumbe wengi kutowaunga mkono watu wenye misimamo thabiti ndani ya chama na badala yake tumekuwa tukitumia rasilimali za chama kuwajenga wajumbe ndio.

Kwa mfano hivi sasa tunapozungumza, wakati katibu mkuu wa chama anasema mjadala wa zitto kabwe umefungwa rasmi, amewaagiza wakurugenzi wa chama kuzunguza nchi nzima kusambaza waraka waliouandaa ukimchafua zitto. Hii si sawa hata kidogo, si vema kutumia rasilimali za chama kuwanufaisha watu binafsi kutimiza matakwa yao ya kisiasa.

Nafsi yangu haipo tayari kuendelea kuwa sehemu ya upotoshaji dhidi ya watanzania wenzangu.

Nafsi yangu inanikataza kabisa kuendelea kufumbia macho maovu yanayoendelezwa na chama changu.

Nafsi yangu imechoka kuendelea kushuhudia ubaguzi wa kidini na kikabila unaofanywa wazi wazi na viongozi wa chama changu.

Nafsi yangu imekataa sasa, haipo tayari tena kuwa kuwadi wa kuwahadaa Watanzania kuyafikia matarajio tunayowapa ambayo kamwe hayafikiki.

Kwa kuwa siamini kwamba kuvuliwa nyadhifa kwa zitto kabwe na dkt kitila mkumbo ni kwa sababu ya waraka wa ushindi, bali ninaamini kuvuliwa kwao ni kutokana na hofu ya uchaguzi, ubaguzi wa kikabila na kikanda. 

Hivyo basi, nikiwa na akili timamu kabisa, leo tarehe 30.11.2013 nimeamua kujivua nyadhifa zangu zote nilizokuwa nazo ndani ya chama.

Sioni tena sababu ya kuendelea kuwa MwanaCHADEMA, sioni tena sababu ya kuwa mwenyekiti wa CHADEMA MKOA WA LINDI, sioni tena sababu ya kuwa KATIBU WA SEKRETARIETI YA KAMATI KUU.

Kwa kuwa vipaumbele vya chadema ni kukijenga chama mikoa ya kaskazini. Basi sisi wananchi wa mkoa wa lindi tunawatakia kila la heri, na kwamba waendelee kukijenga chama chao huko huko waliko.

Nashukuru wote ambao nilifanya nao kazi pamoja katika kutekeleza majukumu yangu.

Ahsante Sana

A.O. CHITANDA

0753418510

MWENYEKITI CHADEMA MKOA LINDI
MJUMBE BARAZA KUU TAIFA
KATIBU OFISI YA KATIBU MKUU- SEKRETARIETI

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[Mabadiliko] Kesho Nitahutubia Kwa Mara Ya Kwanza Kijijini Kwetu Nyeregete...!

Saturday, November 30, 2013 Add Comment
[Mabadiliko] Kesho Nitahutubia Kwa Mara Ya Kwanza Kijijini Kwetu Nyeregete...!
Ndugu zangu,

Matukio mengine ni ya muhimu katika maisha ya mwanadamu. Kesho Jumamosi nitahutubia kwa mara ya kwanza kijijini kwetu Nyeregete. Ni kijiji alichozaliwa baba yangu. Naisubiri kwa hamu siku ya kesho.

Ni kijiji nilichocheza utotoni kila nilipopata likizo ya shule. Na kesho nitasikilizwa na ndugu na jamaa wa kijijini kwetu.

Ni kwenye tukio la harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kikundi cha wanawake kwa ajili ya kujikomboa kiuchumi kwa shughuli za kilimo.

Nitaongea kuhusu elimu na maendeleo. Watu wengi wakiwemo wazee wa kijiji wamealikwa. Na pengine hakuna hotuba ngumu kama ya kuhutubia kijijini kwenu. Si wamesema, nabii hakubaliki kwao.

Natumaini hakuna atakayenirushia yai viza!

Usiku Mwema.

Maggid.
Iringa.

--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 
MUHIMU KWA WANACHAMA WOTE: Jukwaa hili litafungwa hivi karibuni hivyo hii ni taarifa ya Mwisho kwako kuhakikisha unajisajili www.mabadiliko.com
 
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[wanabidii] Man gets 10 years for sleeping with a Goat !!!!

Friday, November 29, 2013 Add Comment
[wanabidii] Man gets 10 years for sleeping with a Goat !!!!
Now this is the kind of news that embarrasses me about our judicial system. A man who sleeps with a goat does not belong in prison. That is a sick man who needs psychiatric treatment; or at best, a woman. Spending hundreds of thousands of shillings on this guy over a 10-yr period is a waste of taxpayers' money, not to mention the possibility that he probably has a wife and children to look after who will now be condemned to artificial poverty. Mtume !!!

That aside; what prompts a grown man to choose to sleep with a goat?  Is it curiosity, lack of a woman or just as I theorize, a mental illness? In this case, the man says he had a disabled wife. could it be that she could not make love to him and instead of cheating on her he chose to do a goat? I hope his appeal makes a difference.
What about the guy who went to relive himself in the bushes and caught this guy? Why can't he be charged with polluting the environment?

http://www.standardmedia.co.ke/?articleID=2000098975&story_title=court-hands-man-ten-years-in-jail-for-sleeping-with-goat

Court hands man ten years for sleeping with goat
Updated Friday, November 29th 2013 at 15:18 GMT +3 0

By Paul Gitau. MALINDI, KENYA:
There was shock and drama at a Malindi court when a magistrate sentenced a middle aged man to ten years in jail after he admitted having sex with a goat.

Members of pubic inside the court room were shocked when the charges were read against Katana Kitsao Gona only for him to admit he committed the offence.

Present in the court was a she goat that the accused was said to have had carnal knowledge of.
Gona was sentenced to serve ten years in prison by the Malindi Resident Magistrate Mrs Muthoni Nzibe.

The accused had been charged that on 25th November 2013 at Dabaso village in Gede location within Malindi district in Kilifi county he had carnal knowledge of a goat.

Prosecuting Chief Inspector Jimmy Kema told the court that on the material day a man had gone to relieve himself in a bush when he saw some clothes hanging on a tree.
Inspector Kema said upon further search to establish the owner of the clothes he spotted the accused having sex with the goat. The witness left and alerted the owner of the goat together with the villagers they later cornered Gona in the act. He was nabbed and handed over to police officers at the Watamu police station.

 Also presented in court was a report from District veterinary officer who indicated that after examining the goat they discovered fluid mucus on the virginal opening of the goat and blood was also oozing from its vulva.

In Mitigation the accused pleaded for pardon saying he had a disabled wife who depended on him.

However the magistrate noted that the offence was serious and sentenced him to serve ten years in prison. He was given fourteen days to appeal.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[wanabidii] TAMKO LA MWANAKIGOMA KUHUSU MGOGORO CDM

Friday, November 29, 2013 Add Comment
[wanabidii] TAMKO LA MWANAKIGOMA KUHUSU MGOGORO CDM
Naendelea na maombi kanisani kuwaombe "busara" viongozi wa chadema
makao makuu a waliovuliwa madaraka bila kuwasahau wanachama wa kwlei
na uongo waliopata kuchangia suala hili tangu lilipoibuka

naanza.......
najua yeyote mwenye busara katika hili ambaye hana chuki yeyote wala
maslahi binafsi kati ya pande hizi mbili

basi hawezi kutoa msimamo wowote unaolenga kumchafua kiongozi aliye
ndani au vuliwa madaraka naona kama hiyo nikivuruga zaidi

jamani haya yametokea kama unadhani huna uchungu na namna chama
kinavyoharibiwa kwa tukio hili basi kaa kimya si lazima uchangie au
utoe msimamo nakuwaaminisha watanzania unavyodhani

tambueni kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi

nadhani busara zitimike kumaliza mgogoro huu bila kuwakumbusha watu na
kuwakalilisha kuhusu udini, ukabila na ukanda vyote hivyo vinafaanya
watu wachukie zaidi chadema ambao tunaona wananchi wengi wanekuwa
wakiamini zaidi katika upinzani.

mambo hayo mnayasema mnaojiita viongoxi vipi katika vikao vya chaka
mmewahi kusema?

kumbikeni nyie viongozi mliapa kuoinda na kutetea chama lakini leo
mmoja anamwaga mbonga mwingine ugali then pande zote mnaona sifa
kuweka hadharani uozo wenu kwani vikao vyenu mlivituiaje?

someni vizuri tahariri ya gazeti la Jamuhuri siku chache zilizopita
tutapata chadema yenye nguvu

Mbowe ni nani! Dk Slaa na Zitto ni nani chadema hawa ni zaidi ya chama?

shida ya viongoxi kuwa na sifa zaidi ya chama ndio hivo hawa watimie
busara ikishindikana wajiuzuru tupate wengine.

tusishindwe kuendesha chama kwa hofu ya kuitwa udini, ukabila,
misimamo, ukanda, nani na wa dini gani alinyimwa fomu kwakuwa ni dini
fulani au mkoa fulani?

hao waliofukuzwa arusha niwa ukanda wa wapi? mbeya au Tabora?
jamani hivi mwenyekiti, katibu mkuu au naibu wake ni nani katika vyama?

kama wajumbe wanapinga jambo kwa wingi viongozi hawa wana mamlaka kwa
nyadhifa zao kupinga? basi wajumbe wanakuwa dhaifu na wajiuzuru kwani
wanaburuzwa na hawafai.

kama vipi wanachamavwenzangu hawa watu hawatufai kwann wao lazima
kugombea? kwani Zitto aliyetumia nguvu nyingi kujenga chama anaona
fahari chama kife kwa sababu binfsi za uenyekiti tena wakati huu wa
kushika dola

kwani Mbowe ameambiwa bila yeye kuendelea kuwa chair chadema haiwi hai?

tunawapa vichwa sana watu hawa nadhani chadema ni taasisi kubwa kuliko hawa

"sisi wanachama tutakuwa wajinga kukimbatia watu hao kwa maslahi yao
binafsi kana kwamba bila wao hakifanyiki kitu, je! wakifa leo chadema
inakufa?"

viongoxi wilayani mikoani ni ujinga kubwa kudhani matsmko yenu kuuga
au kutounga mkono maamuzi ya kamati kuu kuwa yanasaidia chama ni kuuwa

wito cdm makao makuuvangalieni jambo hili kama kuma chuki na fitna
mjiuzuru au malizeni kwa vikao vya muafaka na kwa makubakiano maalimu
ili atakayekiuka basi aadhibiwe

naomba kamati kuu na waliofukuzwa acheni kutunishiana misuri ni aibu
kwenu na chama kwani mwehu akichukua nguo zaki bafuni wwkati unaoga
busara nikumkimbixa ukiwa uchi au unatilia kungoja ndugu jamaa na
marafiki wakuletee nguo ujisitili kisha ufuatilie nguo hizo au uache?

mwisho, huu ni mtihani kwenu kadri mtakavyo limaliza bila
kusambaratisha chama ndivyo tutakavyokuwa na imani na nyie katika
kuelekea kuongoza nchi

tahadhari, hapa ndipo tutamjua anayetumika kuuwa chama kuelekea
uchaguzi mkuu 2015 kati ya makundi hayo

chonde chonde acheni kutumia vibaya media kujidharirisha kwa hayo
tumieni vikao rasmi na visivyo rasmi mmalize

wasalaaam, Mungu ibariki Tanzania ibariki CDM, Amini!!!!!!

Jacob Ruvilo,
mwanachama, kigoma
0787265298

On 11/29/13, Chadema Tanga <mabadilikochadema@gmail.com> wrote:
> *TAMKO LA MJUMBE WA BARAZA KUU , MKUTANO MKUU CHADEMA, MJUMBE WA KAMATI
> TENDAJI YA BARAZA LA VIJANA TAIFA (BAVICHA), MWENYEKITI WA VIJANA MKOA WA
> TEMEKE NA MWENYEKITI WA CHADEMA JIMBO/WILAYA YA TEMEKE KUHUSU MGOGORO NDANI
>
> YA CHAMA NA UAMUZI WA KAMATI KUU KUWAVUA NYADHIFA MJUMBE WA KAMATI KUU
> Dkt. Kitila Mkumbo na NAIBU KATIBU MKUU zitto kabwe *.
> *UTANGULIZI. *
> Mimi Patrick Y.Joseph, ni mwanachama na kiongozi wa Chama cha Demokrasia na
>
> maendeleo CHADEMA ninayeshikilia nyadhifa mbali mbali kwa sasa kama
> inavyoonekana hapo juu kwenye kichwa cha Habari. Ninawashukuru kujitokeza
> kwenu hapa ili tushirikiane kuufikisha ujumbe kwa Watanzania kuhusiana na
> maswala yanayoendelea kwenye chama chetu hivi sasa.
>
> *MIGOGORO NDANI YA CHAMA*
> Chama chetu kimekuwa na tabia ya kuingia kwenye migogoro kila panapokaribia
>
> chaguzi mbali mbali za ndani ya chama, migogoro hii hupelekea mpaka
> kuchafuana na kutukanana miongoni mwetu kiasi cha kuitana wahaini, wasaliti
>
> na wengine kuwaita wenzao wanatumika lengo likiwa ni kuwadhoofisha mbele ya
>
> wanachama na jamii kwa ujumla.
>
> Tumeiona mifano mingi ya namna hii, wakati marehemu Chacha Zakayo Wangwe
> alipotangaza kugombea uenyekiti mgogoro wa namna hii ulijitokeza, aliitwa
> majina yote mpaka anapoteza uhai wake hakuwa akisemwa vizuri kwenye chama,
> hakuchafuliwa na watu walio nje ya chama. Alichafuliwa na viongozi wenzie
> waliotofautiana msimamo.
>
> Alipotangaza zitto kabwe kugombea uenyekiti hali ikawa hiyo hiyo, akaitwa
> msaliti, anatumika na mengineyo mengi, alipotangaza kujitoa kugombea
> akaachwa kidogo apumzike.
>
> Tunakumbuka yaliyotokea wakati wa chaguzi za ubunge wa viti maalum,
> tunakumbuka pia chaguzi za mabaraza ya chama, wakati nagombea nafasi ya
> umakamo mwenyekiti wa vijana nako pia waliogombea uenyekiti waliitwa kila
> aina ya majina.
>
> Kwa kifupi migogoro hii ni ya kutengenezwa ili kudhoofishana kuelekea
> chaguzi za ndani ya chama.
> Hivi sasa tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa chama tumeshuhudia tena
> Zitto Kabwe na Dkt Kitila Mkumbo wakikutana na dhahama hiyo hiyo.
>
> Hali hii si nzuri kuruhusu iendelee kushamiri ndani ya chama maana
> haikijengi chama zaidi ya yote inakibomoa tu.
>
>
>
> *KUHUSU MAAMUZI YA KAMATI KUU*
> Nikiwa kama mjumbe wa Baraza Kuu la chama ninayewakilisha wilaya ya Temeke,
>
> na nikiwa kama mjumbe wa Kamati Tendaji ya Baraza la vijana la Taifa (
> *BAVICHA)*
>
> Nimefadhahishwa sana na uamuzi uliofikiwa na kamati kuu ya chama dhidi ya
> ndugu Zitto kabwe na Dkt. Kitila mkumbo.
> Ukiachilia mbali kwamba kamati kuu haikuwa na mamlaka ya kikanuni wala
> kikatiba kufikia maamuzi iliyoyafikia na kuyatangaza kwa umma.
>
> Lakini imeonyesha ni jinsi gani wametawaliwa na Chuki, Ghadhabu, Unafiki na
>
> Ubaguzi uliopitiliza.
>
> Ni uamuzi ambao hauwezi kuungwa mkono na mwanachama yeyote mwenye akili
> timamu,kwa kuwa haukisaidii chama badala yake unapandikiza chuki miongoni
> mwa wanachama.
> Uamuzi huu uliojawa na hofu kubwa ya kiuchaguzi, hofu ya madaraka na hofu
> ya kupoteza umarufu unapaswa kukemewa na kusababisha watu wenye akili
> timamu wajiulize mara mbili mbili kama ni sawa ama la.
>
> Kwa mantiki hiyo basi, nikiwa kama mjumbe wa baraza kuu, ninatoa masikitiko
>
> yangu kwa kamati kuu kufanya kazi isiyowahusu tena bila kufuata hata kanuni
>
> wala Taratibu zozote za kinidhamu baina ya viongozi.
>
> Ningependa umma utambue kuwa sikubaliani na uamuzi huu kwa kuwa haukidhi
> misingi ya kidemokrasia wala kufuata utawala wa sheria.
>
> Haiingii akilini hata kidogo kwa chama kinachopanga mikakati mbali mbli ya
> kuhinda dola, kuwafukuza na kuwaogopa watu wanaopanga mikakati ya wao
> kushinda uchaguzi ndani ya chama.
>
> Kama ni kweli kupanga mikakati ya uchaguzi ndani ya chama ni uhaini na
> usaliti, basi Operesheni zetu za chama ikiwemo M4C zenyewe zinapaswa kuwa
> uhaini uliopitiliza kwa kuwa nazo ni mikakati ya chama kushika dola.
>
>
> *MSIMAMO WANGU*.
>
> Ninamtaka mwenyekiti akishirikiana na watendaji wengine wa chama waitishe
> mkutano wa dharura wa baraza kuu ili tutolee maamuzi sahihi swala hili.
>
> Ninataka pia pamoja na agenda zitakazojadiliwa,
> *(i).* *watueleze ni kwanini wameamua kusambaza waraka wanaozani
> unawadharirisha kina zitto na mkumbo badala yake waraka huo unakidharirisha
>
> chama kwa kuonyesha madhaifu ya mwenyekiti na katibu mkuu wa chama*.
>
> *(ii). Ni kwanini tusiamini kwamba maamuzi haya yameathiriwa na hofu ya
> chaguzi za ndani ya chama* .
>
> *(iii). Ni kitu gani kimeifanya sekretarieti ya kamati kuu itangaze ratiba
> ya uchaguzi mkuu wa ndani ya chama baada ya kuwachafua miongoni mwa watu
> waliotarajiwa kugombea nafasi mbali mbali mpaka kuwavua uanachama*.
>
> Ni vema sasa tu tukijenge chama chetu bila kufuata maswala ya ubaguzi wa
> kidini na kikabila ama kikanda.
>
> Chama chetu kimekuwa kikishtakiwa sana kuhusiana na matatizo ya kidini na
> kikabila, lakini pia chama chetu kimekuwa kikiwatumia Zitto na Arfi kama
> ishara ya kutokuwa na udini ndani ya chama, sasa inawezekanaje kuwatimua na
>
> kuwaita wasaliti watu ambao mmekuwa mkijivunia.
>
>
>
> Mwisho ninapenda kusema kuwa huu ni msimamo wangu na kwamba sipo tayari
> kuburuzwa wala kuruhusu kuona tunaendelea kuibomoa demokrasia
> tunayoitangaza kila kukicha.
>
> Nitaendelea kuwa mwanachama mtiifu wa chama changu, na kukishauri namna
> bora ya kuendeleza demokrasia ndani ya vikao na sita ogopa kueleza maoni
> yangu kwa Watanzania.
>
> Nawashukuru sana.
>
> Imetolewa na ;-
>
> *Joseph* *Y.*
> *Patrick*
>
> +255713802226
>
>
> Mwenyekiti wa chadema wilaya/jimbo Temeke
> Mwenyekiti BAVICHA mkoa wa Temeke
> Mjumbe wa Baraza Kuu la Chadema Taifa
> Mjumbe wa mkutano mkuu wa Chadema Taifa
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups
> "Wanabidii" group.
> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an
> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
>

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

[wanabidii] Sera Ya Gesi

Friday, November 29, 2013 Add Comment
[wanabidii] Sera Ya Gesi
Ndugu Wanabidii,

Nimemsoma Reginald Mengi akisemea kupitia gazeti la Mwananchi la leo kuhusu sera ya Gesi. Mimi binafsi ninakiri kuwa anachosema kuhusu ushirikishwaji wa wananchi kina maana. Je Sera ya Gesi iliyozinduliwa hivi karibuni ina manufaa kwa Wazalendo kama ndio kwa vipi kama sivyo kwa vipi? Je tunahitaji Sera mbadala ambayo itaeleza bayana kwamba wananchi watashiriki kwenye shughuli za gesi kuanzia utafutaji, na uchimbaji, usafirishaji, uhifadhi na uuzaji jumla?

Naomba michango yenu ili tuweze kujenga hoja kwa Serikali yetu ambayo tunaamini ni sikivu.

Ahsante


Herment A. Mrema

[wanabidii] World AIDS Day 2013: Statement by Donald Kaberuka, President of the African Development Bank Group

Friday, November 29, 2013 Add Comment

If you cannot read that message, click here.

 

 

PRESS RELEASE

 

World AIDS Day 2013 Statement by Donald Kaberuka, President of the African Development Bank Group

 

World AIDS Day is December 1

 

TUNIS, Tunisia, November 29, 2013/ -- Africa has made significant progress in fighting the HIV/AIDS pandemic. In the past seven years, AIDS-related deaths declined by 32%.The number of people contracting the HIV infection declined by 25% in the past 10 years. The rate of mother-to-child transmission of HIV has also declined from 35% in 2001 to 26% in 2010. Ten years ago, we had fewer than 50,000 people on ARV treatment; today we have over 6 million receiving treatment. A few years ago, Senegal and Uganda were the only success stories for their outstanding results and containment of HIV; now we have 25 countries that lowered HIV infections by more than 50%. A lot has been achieved; however, the risks are far from over. Indeed, new infections are a threat. It is time to raise, not to lower our vigilance.

 

Photo Donald Kaberuka: http://www.photos.apo-opa.com/plog-content/images/apo/photos/donald-kaberuka-afdb-president.jpg

 

Recall, 30 years ago, when the first HIV-positive case was reported; 24 million Africans have lost their lives. Africa still bears the heaviest burden of the disease globally and accounts for 91% of the world’s children with HIV, 89% of HIV orphans and 69% of people living with HIV. Each day, 3,500 Africans die of AIDS and millions of others and their families and communities go through economic, psychological and social traumas. HIV-related stigma still hurts people, in society, in their workplaces and homes. Women in Africa are more severely affected than men. In 2012, 58% of people living with HIV were women.

 

HIV/AIDS continues to have a huge detrimental impact on the most important resource of our continent: our people. It robs the continent of vitally needed skilled workers and deprives families of their incomes. It has hampered our ability to educate and build our human capital. Kenya lost an estimated 1.7% of its teachers between 2000 and 2010 due to HIV/AIDS.

 

For the African Development Bank, in partnership with governments, international organizations, civil society and the private sector, the future of HIV/AIDS agenda is about ‘getting to zero’. Zero new HIV infections, zero discrimination and zero AIDS-related deaths. Getting there is not easy and the Bank aims to support African countries to, first, take ownership of the AIDS response. It is time for Africa to take bold steps to reduce dependence on external donors and work towards more sustainable domestic solutions. According to UNAIDS, Africa will require between US $11 billion and $12 billion for its AIDS response by 2015. Yet international funding to HIV is dwindling, putting our progress at risk.

 

Second, the Bank supports African countries in increasingly applying ‘value for money’ and ‘solidarity’ principles to strengthen social systems. The way HIV resources are mobilized and spent needs to change. The vertical approach may no longer be appropriate and cost-effective in many contexts. There is a need to mainstream AIDS-related services into the general healthcare delivery systems and to support the local production of ARVs.

 

Third, the Bank supports the building of inclusive health systems to fight stigma and discrimination. Let us all tackle stigma and discrimination by building a supportive and caring culture both in their communities and workplaces. We cannot leave the victims of HIV/AIDS and their families behind.

 

Finally, the Bank, through its inclusive growth agenda, aims to support the reduction of women’s increased vulnerability and prevent mother-to-child HIV transmission. Addressing the gender dimension is an important priority in the response to the epidemic. Recent progress suggests that the solutions are in our hands. We can reduce gender inequalities by empowering women with information and services to prevent and treat HIV. Strategies to counter and manage gender-based violence can be effectively included in HIV-prevention programs. Effective treatment to reduce mother-to-child HIV transmission now needs to be scaled up and made accessible to those who need them, regardless of their socioeconomic status. Training health workers to provide gender-friendly counseling and services must also be prioritized. Most importantly, we need to sensitize men and elicit their involvement to create a supportive environment for reducing women’s vulnerabilities to the epidemic.

 

Getting to zero starts with us. It is time for Bank staff to take care of themselves and their families by taking advantage of HIV/AIDS services the Bank’s Medical Centre provides. These include Anonymous Voluntary Confidential Counseling and testing available to all Bank staff and their families.

 

I also want to stress that the African Development Bank is a workplace of zero discrimination and that we must support each other in our communities and workplace. Our fight to get to zero is producing results. Let’s continue in order to give the next generation of Africans – our children, our sons and daughters -- an AIDS-free life ahead. Zero has a value!

 

Donald Kaberuka, President of the African Development Bank Group

 

Distributed by APO (African Press Organization) on behalf of the African Development Bank (AfDB).

 

SOURCE 

African Development Bank (AfDB)

 

Safe Sender Instructions

 

UNSUBSCRIBE